TTCL

EQUITY

Tuesday, January 12, 2016

Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein asisitiza kurudiwa kwa uchaguzi Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohamed Shein amesema mazungumzo ya kutatua mgogoro wa kisiasa Zanzibar yanaendelea na hayajasita ingawa amesisitiza kuwa marudio ya uchaguzi mkuu zanzibar upo na utarudiwa.

Dr Shein ambaye mara baada ya kuwasili uwanjani alikagua Gwaride la heshima liliondaliwa na vikosi vya ulinzi na uslama vya jamhuri ya muungano wakiwemo JWTZ na polisi na vikosi vya SMZ ambapo akitoa msimamo huo wa serikali katika hotuba yake kwa wananchi wa Zanzibar katika siku ya kilele cha sherehe za miaka 52 ya mapinduiz ya Zanzibar zilizofanyika uwnaja wa Amani na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi wakiwemo viongozi wa serikali zote mbili wakiongozwa na rais John Magufuli, waziri mkuu kassim Majaliwa, makamu wa rais Samia Suluhu, marais wastaafu wa muungnao Ali Hassan Mwinyi, Benjamini Mkapa na Jakaya Kiwete pamoja na rais mstaafu wa Zanzibar Dr Amani Abeid Karume na viongozi waandamizi wa serikali zote mbili.
 
Rais wa Zanzibar katika hotuba yake hiyo kwa wananchi alizumgumzia suala la amani na utulivu wananchi na kuahidi kuhakiksha suala la amani inalindwa wakati wote huku pia akisisitiza kuwa muungano wa Tanznaia utalindwa kwa nguvu zote kwa vile upo kikatiba na sheria ambapo pia alizungumzia suala la uchumi wa Zanzibar.
 
Mapema makamu wa pili wa rais Balozi Seif Ali Iddi amesema mapinduzi ya 1964 ni kigezo cha wazanzibari kuwa huru katika nchi yao na ishara ya wazanzibari kuondoa utawala uliokuwa ukiwakandamiza wananchi hivyo daima yatalindwa.
 
Mapema Dr Shein alipokea maandamano ya wananchi wa mikoa mitano ya Zanzibar na pia wafanyakazi wa wizara na taasisi za serikali ya Zanzibar na muungano na pia  kushuhudia kikosi cha makomandoo wa JWTZ wakipita kikakamavu na kivita ambao walipita mbele ya jukwaa kuu na pia kushuhudia Gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama  vilivyopita  kwa mwendo wa kasi na pole.

No comments:

Post a Comment