Akizungumza katika ziara yake aliyoifanya katika hifadhi ya taifa
ya Serengeti na kushuhudia idadi kubwa ya mifugo, mazao na baadhi ya
wananchi wakidiliki kujenga ndani ya alama za mwisho wa hifadhi hiyo
huku wakijua kufanya hivyo ni kosa naibu waziri wa maliasili na utalii
Mhe Mhandisi Ramo Makani amemwagiza mkurugenzi mkuu wa hifadhi za
taifa-TANAPA kuwakilisha mara moja rasimu mpya ya mapendekezo ya
mabadiliko ya sheria kwa kuboresha kipengele cha adhabu ili ziendane na
thamani ya uharibifu unao fanyika.
Wakati huohuo Mhe Ramo amezungumzia mikakati ya serikali ya awamu ya 5 ya kupambana na ujangili hususani wa Tembo.
Katika taarifa yake mhifadhi mkuu wa hifadhi ya taifa ya
Serengeti-TANAPA ameitaja changamoto kubwa inayoikabili hifadhi hiyo
yenye adhi ya kimataifa ni ujangili ambao umekuwa ukiongezeka mwaka hadi
mwaka ambapo katika kipindi cha mwaka 2014-2015 wahalifu zaidi ya elfu 1
na jumla ya bunduki 109 zikiwemo slaa nzito aina ya SMG zikikamatwa.
No comments:
Post a Comment