TTCL

EQUITY

Wednesday, January 13, 2016

Brightermonday yamulika changamoto za ajira Tanzania

DSC_0955
Kampuni ya BrighterMonday ambayo ni tovuti namba moja ya ajira nchini Tanzania. Leo hii imezindua kituo kipya ambacho kitatumika kwa ajili ya huduma ya mawasiliano na wateja ambao ama ni watafuta ajira wapya au wanataka kubadili ajira.

Akizungumza wakati wa hafla ya kifungua kinywa Bwana Lugendo Khalfan, Meneja Masoko wa Kampuni ya BrighterMonday Tanzania alisema kwamba changamoto kubwa nchini Tanzania ni kuwa kuna watafuta ajira wengi sana kuliko nafasi za ajira zilizopo sokoni, hivyo kwa kupitia kituo hiki itawarahisishia watafuta ajira kuongeza nafasi ya kupata ajira kiurahisi na huduma zote ni bure.
Naye Bi. Eva Slootweg, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya BrighterMonday amekielezea kituo hicho cha ajira ambacho kipo katika tovuti ya kampuni hiyo ambayo ni www.brightermonday.co.tz kuwa kina mfumo wa kuchambua maombi ya kazi mpaka kupata wachache wenye kukidhi viwango.
Kwenye suala la upatikanaji wa watu wenye vigezo, utendaji mzuri, mahusiano kazini na ujuzi katika uongozi pamoja, kampuni ya Brighter Monday ina uwanja mpana ambao unakwenda sambamba na mabadiliko yaliyoko katika sekta ya ajira ambayo si tu inatilia mkazo uwezo wa utendaji kazi na ufanisi wa mwombaji ajira bali ni kwa namna gani mwomba ajira anaendana na utamaduni wa taasisi husika.
Bi Sabiha Monji, Mkurugenzi Mtendaji wa Shugulika Recruitment, alisema mojawapo ya changamoto wanayokutana nayo hapa Tanzania ni kukosa umakini kwa baadhi ya watafutaji ajira, “wengine wanashindwa kufika katika usaili bila hata kutoa taarifa”. Katika utafutaji kazi katika mtandao, Bi Sabiha alidokeza kwamba Tanzania kwa sasa ina watafuta ajira zaidi na zaidi wanaotafuta kupitia mtandao, hivyo kuna kuna ongezeko la watumiaji mtandao katika kutafuta ajira.
Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya waajiri 3000 kutoka sekta mbalimbali huajiri kupitia BrighterMonday.
Kampuni ya BrighterMonday inafahamu changamoto zinazowakabili wadau wake hivyo hutoa ufumbuzi unaokidhi matakwa ya mwajiri kwa kumpatia mwajiriwa anayewafaa. Kutokana na uzoefu wa muda mrefu na kutokana na maoni kutoka kwa wateja, na kwa ubunifu wameweza kuongoza soko la ajira nchini.
Kampuni ya BrighterMonday inadhamiria kuendelea kuwashirikisha wadau wake kwa njia ya mijadala ya kiuongozi ili waelewe changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya ajira Tanzania na kutoa suluhisho kwa ubunifu na mikakati iliyo bora kama  mshirika na kampuni namba moja ya ajira nchini.
Brighter Monday ni nini?
BrighterMonday Tanzania ni kampuni kubwa ya ajira mtandaoni, yenye watafuta ajira bora kuliko kampuni yoyote. Kwa nia ya kuwarahisishia watafuta ajira, tumeshirikiana na waajiri mbalimbali kuhakikisha kuwa katika upatikanaji wa ajira kirahisi Zaidi, na ni daraja kati ya soko la ajira na waajiri. BrighterMonday iko chini ya mwamvuli wa makampuni ya One Africa Media (OAM), kampuni kubwa ya biashara za mtandaoni barani Africa. OAM inashughulika na safari za kiutalii mtandaoni, magari na ajira katika maeneo mbali mbali Afrika.

No comments:

Post a Comment