Mkurugenzi asiye mtendaji wa kampuni ya ndege ya Fastjet Balozi Ami
Mpungwe, akizungumza na wasafiri wakati wa kuanzisha safari za ndege
hiyo kwenda Nairobi kutokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam, kutoka kulia ni
Mkurugenzi asiye mtendaji Lawrence Masha, Meneja mkuu wa kampuni hiyo
(Afrika Mashariki) Jimmy Kibati na Meneja wa mahusiano kati ya Fastjet
na Serikali, Mhandisi August Kowero.
Meneja mkuu wa Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati na crew yake
wakishuka kwenye ndege baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Jomo Kenyatta.
Balozi
wa Tanzania nchini Kenya, John Haule (kulia) akikata utepe ili
kuikaribisha ndege ya Fastjet nchini Jijini Nairobi mara baada ya ndege
hiyo kutua katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jana, kushoto
kwake ni Meneja mkuu wa Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati na
Mkurugenzi asiye mtendaji balozi Ami Mpungwe.
Wageni
mashuhuri wakishirikiana na viongozi wa Fastjet kukata keki mara baada
ya ndege kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta
jijini Nairobi jana, kutoka kushoto ni Meneja mkuu wa Fastjet Afrika
Mashariki Jimmy Kibati, mkurugenzi asiye mtendaji Ami Mpungwe, Balozi wa
Tanzania nchini Kenya John Haule, Mkurugenzi asiye mtendaji Lawrence
Masha na Meneja Masoko na Maendeleo ya Biashara wa Mamlaka ya Viwanja
vya ndege nchini Kenya (KAA) William Simbah.
Picha ya pamoja.
Kampuni ya
ndege ya Kiafrika yenye gharama nafuu fastjet,imepanua mtandao wake wa
safari barani Afrika kwa kuwa na safari za kimataifa za kila siku
kutoka Dar es Salaam na Kilimanjaro kwenda Nairobi na hali kadhalika
safari za ndani za kila siku kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar.
Uzinduzi wa
safari za anga za fastjet kutoka Dar es Salaam hadi Nairobi,
Kilimanjaro hadi Nairobi na Dar e s Salaam kwenda Zanzibar zote
zimefanyika Januari 11, 2016 na hivyo kufanya iwe ni hatua muhimu katika
kujipanua katika safari zake kimataifa na kitaifa.
Safari za
kila siku kwenda Zanzibar zinatarajiwa kuwarahisishia watanzania walio
wengi pamoja na wageni wa kimataifa kuitembelea Zanzibar,kukuza utalii
na biashara pamoja na kuchangia kwa kiwango kikubwa kwenye kukua kwa
uchumi visiwani humo.
Kuzinduliwa
kwa safari za fastjet kwenda Nairobi kutoka Dar es Salaam kunaanzisha
enzi mpya ya abiria ambao wamekuwa wakitaabika kwa tozo kubwa ya nauli
kwa usafiri wa anga kati ya nchi mbili za Afrika Mashariki ambazo
uchumi wake unakua kwa kasi.
Matokeo ya
safari za fastjet nchini Kenya tayari yameshaanza kujadiliwa,
yakikolezwa na ukweli kwamba nauli dhidi ya mashirika washindani
yanayofanya safari kati ya nchi hizi mbili ambako ni kushuka kwa kasi
hadi ya asilimia 40 siku ya kwanza tu tangu fastjet ilipotangaza kuanzishwa kwa safari zake kati ya Kenya na Tanzania.
Meneja Mkuu
wa fastjet Tanzania John Corse anasema, “ukweli ni kwamba ushindani ni
mzuri kwa abiria. Unaleta nafasi kuchagua jinsi ya kusafiri na pia
unasababisha nauli kushuka.”
Nauli za
fastjet kimsingi ziko chini kuliko nauli zinazotozwa na mashirika
mengineya ndege ambayo hivi sasa yanafanya safari kati ya Tanzania na
Kenya ambapo nauli za fastjet kutoka
Kilimanjaro/Nairobi ni kuanzia dola 50 kw safari moja na ya kwenda Dar es Salaam/Nairobi
ni dola 80 kwa safari moja. Nauli hizo hazijumuishi kodi za serikali ambazo ni dola
49kwa kuondokea Tanzania na dola 40 kwa kuondokea Kenya na hivyo fastjet
kuwashauri abiria kukata tiketi zao mapema ili kuitumia fursa hiyo ya nauli ya bei
nafuu. fastjet inatarajia kuongeza safari moja zaidi kwenye niia yake mpya ya Kenya
kutokan
ana mahitaji ya wateja kuongezeka kutokana na kumudu, usalama, kasi na
huduma kwa wakati na tayari imeshaonesha kwamba inatarajia kuzindua
safari kati ya
Zanzibar na Nairobi na hali kadhalika kati ya Dar es Salaam na Mombasa baadaye mwaka huu 2016.
“Kama
ambavyo imekuwa kwa njia zetu nyingine ambazo fastjen timezindua
tunatarajia abiria wetu walio wengi kwenye njia yetu mpya Kenya kuwa
abiria wa kwanza ambao huenda wasingemudu kusafiri kwa njia ya anga
hapo awali,” anabainisha Corse.
Matarajio haya yanaungwa mkono na utafiti uliofanywa na fastjet ambao unaonesha
Kuwa zaidi
ya theluthi moja ya abiria watakuwa wanasafiri kwa ndege kwa mara ya
kwanza na hali kadhalika kumudu usafiri huo kwa mara ya kwanza.
“Usafiri
wa anga ambao abiria wanaumudu ni msingi wa kukua kwa uchumi barani
Afrika kutokana na matokeo chanya yanayosababishwa na bei nafuu ya
usafiri wa ndege kwa maisha ya wananchi na uchumi kwa jumla,”alisema
Corse.
“Tunazishukuru
wizara za usafirishaji na mamlaka za usafiri wa anga za Tanzania na
Kenya kwa kufanya kazi pamoja kuwezesha fastjet kutambua dira yetu ya
kuongezeka kwa idadi ya wateja ambao wanaweza kufikia usafiri wa anga
wanaoumudu,” alihitimisha Corse.
Jambo
ambalo lina umuhimu zaidi kwenye njia hii mpya ni njia mbadala ya
kuibeba mizigo inayojulikana kama “freighty” ambayo inaruhusu abiria
kusafiri na mzigo hadi kilo 80 kwenye mabegi kwa dola 80. Mbadala huu
wa mzigo kimsingi unatarajiwa kuwa maarufu kwa wafanya biashara
wanaosafiri na fastjet kununua bidhaa za jumla na kuzisafirisha kwa
ajili ya kuuzakwenye masoko ya ndani. Ukataji tiketi unaweza kufanyika
kupitia mtandao wa www.fastjet.com, kupitia wakala waliothibitishwa na fastjet au kwa njia ya mawasiliano ya simu: +255-784-108900. Malipo ya tiketi yanaweza kufanyika kwa fedha taslim, kwa njia ya mtandao au kupitia malipo kwa njia ya simu.
RATIBA
Nairobi kwenda Dar es Salaam | Kuondoka | Kufika |
Kila siku 8:40 | 10:05
Dar es Salaam kwenda Nairobi | Kuondoka | Kufika |
Kila siku 3:50 | 5:10
Nairobi kwenda Kilimanjaro | Kuondoka | Kufika |
Kila siku 5:40 | 6:40
Kilimanjaro kwenda Nairobi | Kuondoka | Kufika |
Kila siku 7:10 | 8:10
Dar es Salaam kwenda Zanzibar | Kuondoka | Kufika |
Jumanne, Jumatano, Alhamisi, Jumamosi na Jumapili | 2:30 | 3:00 |
Kila siku 1:10 | 1:40
Zanzibar kwenda Dar es Salaam | Kuondoka | Kufika |
Kila siku 2:10 | 2:40
No comments:
Post a Comment