TTCL

EQUITY

Tuesday, December 22, 2015

TTCL KUONGEZA UFANISI WA MASAFA YA MTANDAO, SASA IMEKUJA NA 4G LTE

Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) imezindua rasmi teknolojia ya Long Term Evolution (LTE) inayojulikana kwa jina la mtandao wa 4G. Awamu ya kwanza inayoanza leo siku ya uzinduzi itatoa huduma katika maeneo 11 Jijini Dar es salaam.
Maeneo hayo ni pamoja na  Uwanja wa Ndege wa Mwl J.K. Nyerere, Pugu Road, Posta Mpya, Upanga, Kinondoni, Ubungo, Oysterbay, Mwenge, Mbezi Tangibovu,  Mbezi Exchange, Kunduchi Salasala na Wazo Tegeta.  Awamu pili itakuwa kupeleka mawasiliano hayo katika maeneo mengine ya Jiji la Dar Es Salaam na kasha kusambaa kote nchini.
Huduma hii itaambatana na vifurushi ambavyo vya intaneti vilivyoboreshwa zaidi kulingana maisha ya mtanzania. Mafanikio haya ya kuboresha teknolojia na vifurushi vya intaneti vitarahisisha mawasiliano miongoni mwa wananchi na kukuza matumizi ya TEHAMA nchini. Aidha, kuanza kwa huduma za 4G LTE ya TTCL kutakamilisha nia ya siku nyingi ya Kampuni ya kuwahudumia kikamilifu wateja katika nyanja zote za mawasiliano(Fixed& mobile convergence).
Faida za Mtandao wa 4G LTE
Mtandao huu wa 4G-LTE utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuongeza kasi ya shughuli za maendeleo kijamii na kiuchumi, kuchangia katika kukuza Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, kuongeza uzalishaji katika sekta mbalimbali za maendeleo.
TTCL tunaamini kuwa Mtandao wa 4G- TTCL utafungua fursa pekee katika kukuza sekta ya elimu nchini kwa njia ya mtandao( E education). Ubora wa intaneti hii itatoa fursa kwa wanafunzi, walimu, wakufunzi, wataalamu na wanazuoni kutumia teknolojia katika kujifunza mambo mbalimbali ya kitaaluma na nje ya taaluma.
Mtandao wa 4G LTE utaongeza fursa katika sekta ya Afya ambapo hospitali, vituo vya afya, vyuo vya afya na wadau mbalimbali wataweza kutumia mtandao huu katika kuongeza ufanisi wa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi kwa haraka na uhakika zaidi. Kiwango cha spidi ya intaneti ya 4G kina uwezo wa kufanikisha kikamilifu programu za kutoa huduma za afya kwa mtandao (Telemedicine).
Aidha, mtandao huu pia utanufaisha sekta nyingine za kiuchumi kama vile sekta ya Biashara. Wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa wanahitaji mawasiliano ya ukakika katika shughuli zao. Mtandao huu wa 4G-LTE utakuwa mkombozi wao, na utaleta mageuzi katika kuongeza uzalishaji, kupanua wigo wa masoko ya bidhaa kwa wakulima, masoko kwa wajasirilimali, masoko kwa makampuni ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. 
Pamoja Tunaweza, TTCL- huleta watu Karibu.

No comments:

Post a Comment