TTCL

EQUITY

Tuesday, December 1, 2015

Niyonzima, Tuyisenge na Kizimana washirikiana kuivua Ubingwa Kenya, Full Time ya CECAFA Dec 1 2015 …

December 1 hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Challenge 2015 iliendelea kwa timu ya taifa ya Rwanda ikiongozwa na mchezaji wa Dar Es Salaam Young African Haruna Niyonzima kucheza mchezo wao na timu ya taifa ya Kenya, ikiwa ni siku moja toka Kilimanjaro Stars itolewe na mwenyeji wa mashindano hayo Ethiopia kwa mikwaju ya penati.

amavubi1_l643_h643
December 1 imekuwa zamu ya timu ya taifa ya Kenya kuaga michuano hiyo kwa mikwaju ya penati baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare 0-0, kwa mujibu wa sheria ya mashindano hayo dakika 90 za michezo ya robo fainali ikimalizika bila kupata mshindi inapigwa mikwaju ya penati kupata mshindi.

1407020336amavubi-players
Rwanda wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa jumla ya penati 5-3, mikwaju ya penati ya Haruna Niyonzima, Tuyisenge na Kizimana ilisaidia Rwanda kutinga hatua ya robo fainli ya michuano hiyo, kwa matokeo hayo ni rasmi Kenya ambao walikuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo wamevuliwa ubingwa.

No comments:

Post a Comment