Maelfu ya watu wameandamana katika miji mikuu ya Afrika Kusini wakitaka kutimuliwa kwa Rais Jacob Zuma.
Wanasema visa vya ufisadi na mapendeleo vimeongezeka sana.
Makundi yaliyoandaa maandamano hayo yamekuwa yakitumia kitambulisha mada #zumamustfall kutafuta uungwaji mkono mtandaoni.
Maandamano
hayo yamefanyika Siku ya Maridhiano, siku ya mapumziko ambayo lengo
lake ni kuleta pamoja watu wa asili mbalimbali Afrika Kusini.
Mwandishi
wa BBC Karen Allen aliye nchini humo anasema amekutana na mmoja wa
walioshiriki maandamano dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi 1976.
Anasema maandamano hayo ni kama “mwanzo wa jambo”.
Amesema hiyo ni mara yake ya kwanza kushiriki maandamano tangu wakati huo.
Bintiye mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nodel Askofu Desmond Tutu naye amejiunga na wanaomtaka Rais Jacob Zuma ang’atuke.
Amenukuliwa na tovuti ya habari la DispatchLive akisema: "Huwa twawachagua viongozi wetu na tunaweza kuwang’atua.”
Mpho Tutu ameambia mkutano mkubwa wa #ZumaMustFall mjini Cape Town kwamba wanataka ufisadi nchini humo ukomeshwe.
Wakosoaji wa Rais Zuma wanasema ufisadi umezidi chini ya utawala wake.
Amekanusha vikali madai hayo.
Leo
Bw Zuma, akiongoza sherehe za kuadhimisha Siku ya Maridhiano, ameahidi
kukabiliana na ukosefu wa usawa miongoni mwa watu wa asili mbalimbali.
Hakuzungumzia maandamano dhidi yake.
No comments:
Post a Comment