Kasi waliyoanza nayo Kasi waliyoanza nayo Rais John
Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ambao wanaweza kupewa jina la
‘M kipeo cha pili’ (M2) ya kutumbua majipu ya mafisadi na wakwepa kodi,
huenda ikaibua upinzani ndani ya CCM.
Hofu imetanda miongoni mwa baadhi ya wana CCM na wale wa kambi ya
upinzani wasiopenda mabadiliko na ambao kwa namna moja au nyingine
huenda maslahi yao binafsi yataguswa na kasi hiyo. Katika mazingira
yasiyokuwa ya kawaida wanachama hao wanaangalia namna ya kudhoofisha
juhudi hizo zilizoanzishwa na Rais Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa.
Adui wa kwanza anatoka ndani ya chama chake (CCM) na wa pili
anaibuka kutoka kambi ya upinzani. Shabaha ya vita hivi huenda ni kutaka
kuhujumu nguvu za Rais Magufuli na ili operasheni hii isije kuwagusa na
kuwaumiza vigogo wa pande zote mbili.
Nikianza na adui wa ndani, itakumbukwa kwamba katika kipindi cha
kampeni, kambi zote mbili zilikuwa na ajenda kuu ya “mabadiliko” hata
hivyo dhima ya kupinga ufisadi na rushwa ilikuwa ni shabaha kubwa ya
wapinzani.
Tangu Rais Mafuguli achukue uongozi, mara moja alianza kuonyesha
dhamira yake kwa vitendo pale alipofanya ziara ya kushtukiza katika
Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili na Wizara ya Fedha. Kwenye ziara hizo
alimuondoa Kaimu Mkurugenzi wa Muhimbili, Dk. Hussein Kidanto na
kusitisha bodi nzima ya wakurugenzi.
Siku chache baada ya Rais Magufuli kuacha kilio kwenye ziara yake,
Waziri Mkuu alifuata nyayo na kuzitembelea ofisi za Mamlaka ya Mapato
(TRA), ambapo matokeo yake yalikuwa ni kusimamishwa kazi kwa makamishna
watano akiwamo Kamishna Mkuu wa TRA Rished Bade, baada ya kugundulika
ufisadi mkubwa wa kukwepa kodi kwenye makotena yanayopita bandarini.
Kutokana na hatua hizo za Rais Magufuli za kuanza kutumbua majipu,
kunahofu huenda atawagusa baadhi ya wana CCM. Kuna hofu kuwa ndani wapo
baadhi ya wananchama wasiokuwa waaminifu ambao wameanza kujenga hoja
kuwa endapo hatadhibitiwa mapema, basi mambo yatakwenda mrama kwani
chama hicho kimekuwa kikinufaika na misaada kutoka kwa wafadhili
wanaokabiliwa na tuhuma za ukwepaji wa kodi.
Inahofiwa Rais Magufuli asipodhitibiwa mapema na chama, ipo siku
ataingilia makampuni yaliyoanzishwa na chama siku za nyuma na kuhusishwa
na ufisadi, kwa mfano Meremeta.
Inahofiwa kuwa rungu lake likifikia maeneo hayo, CCM itakuwa
imevuliwa nguo na kwamba hakuna kiongozi wa CCM atakayesalimika pale
atakapoanza kutumbua jipu la makampuni hayo na yale yaliyoanza kusaulika
mfano kashifa ya akaunti ya madeni ya nje (EPA).
Kwa msingi huo, vita vilivyoanza ndani ya chama hicho ni kutaka
kumfunda Rais Magufuli ili asichokonoe yaliyopita. Kwanza aanzie hapa
alikoishia mtangulizi wake. Asahau yaliyopita vinginevyo atatumbua
makovu ya majipu ambayo huenda hata yeye akashindwa kumpata daktari wa
kuyatibu.
Ninachotaka kusema ni kwamba kuna baadhi ya viongozi ndani ya CCM
ambao walihusika kwa njia moja au nyingine kutoa vibali na ‘vimemo’ kwa
wafanyabiashara wakubwa ambao wamekuwa wakivitumia kukwepa kulipa kodi
za serikali kwa maslahi binafsi. Hivyo kasi hii ya Rais itawaumbua
hadharani.
Kwa kutambua hali hiyo, vigogo hao wameanzisha ushirika bubu na
kambi ya upinzani ili kwa pamoja watafute mbinu za kuhujumu nguvu hizo
za Rais Magufuli. Wanadai eti hatafanikiwa bila ya kuungwa mkono na wana
CCM wenzake.
Vita vya pili vinahusu kambi ya upinzani. Mtoa taarifa alisema
kwamba, kambi ya upinzani nako hakuna usalama. Inaelezwa kuwa wapo
baadhi ya vigogo waliopo kambi hiyo ya upinzani ambao pia wana mahusiano
na wakwepa kodi.
Inasemekana baadhi ya viongozi kutoka kambi ya chama tawala
wanawapa nguvu wapinzani ili wamchefue Rais Magufuli kwa madai kwamba
anafanya kazi ya “One man show” yaani kazi bila ushirikiano na wenzake.
Kuna madai kuwa Rais Magufuli haambiliki, hashauriki, hasikii ya
mtu, hivyo anaweza kuleta madhara kwa taifa. Kauli mbiu yao ni kufuta
agenda ya mabadiliko na mbadala wake kuingiza agenda ya “katiba mpya” na
kutangazwa kwa matokeo ya Zanzibar.
"Jamaa atalazimika kujieleza kwenye kelele za wapinzani hivyo
agenda yake ya mabadiliko itakufa tu” alisema mtoa taarifa. Kimsingi
vita hivi vinataka kumtoa Rais Magufuli nje ya reli ili aachane na hoja
ya kutumbua majipu. Hata hivyo, wapiganaji wa vita hivyo wanaogopa nguvu
za Umma iliyopo nyuma. Tusubiri.
Mawasiliano:0713 399004/0767
399004,"mailto:jmkibasso@gmail.com" jmkibasso@gmail.com , ambao
wanaweza kupewa jina la ‘M kipeo cha pili’ (M2) ya kutumbua majipu ya
mafisadi na wakwepa kodi, huenda ikaibua upinzani ndani ya CCM.
Hofu imetanda miongoni mwa baadhi ya wana CCM na wale wa kambi ya
upinzani wasiopenda mabadiliko na ambao kwa namna moja au nyingine
huenda maslahi yao binafsi yataguswa na kasi hiyo. Katika mazingira
yasiyokuwa ya kawaida wanachama hao wanaangalia namna ya kudhoofisha
juhudi hizo zilizoanzishwa na Rais Magufuli na Waziri Mkuu Majaliwa.
Adui wa kwanza anatoka ndani ya chama chake (CCM) na wa pili
anaibuka kutoka kambi ya upinzani. Shabaha ya vita hivi huenda ni kutaka
kuhujumu nguvu za Rais Magufuli na ili operasheni hii isije kuwagusa na
kuwaumiza vigogo wa pande zote mbili.
Nikianza na adui wa ndani, itakumbukwa kwamba katika kipindi cha
kampeni, kambi zote mbili zilikuwa na ajenda kuu ya “mabadiliko” hata
hivyo dhima ya kupinga ufisadi na rushwa ilikuwa ni shabaha kubwa ya
wapinzani.
Tangu Rais Mafuguli achukue uongozi, mara moja alianza kuonyesha
dhamira yake kwa vitendo pale alipofanya ziara ya kushtukiza katika
Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili na Wizara ya Fedha. Kwenye ziara hizo
alimuondoa Kaimu Mkurugenzi wa Muhimbili, Dk. Hussein Kidanto na
kusitisha bodi nzima ya wakurugenzi.
Siku chache baada ya Rais Magufuli kuacha kilio kwenye ziara yake,
Waziri Mkuu alifuata nyayo na kuzitembelea ofisi za Mamlaka ya Mapato
(TRA), ambapo matokeo yake yalikuwa ni kusimamishwa kazi kwa makamishna
watano akiwamo Kamishna Mkuu wa TRA Rished Bade, baada ya kugundulika
ufisadi mkubwa wa kukwepa kodi kwenye makotena yanayopita bandarini.
Kutokana na hatua hizo za Rais Magufuli za kuanza kutumbua majipu,
kunahofu huenda atawagusa baadhi ya wana CCM. Kuna hofu kuwa ndani wapo
baadhi ya wananchama wasiokuwa waaminifu ambao wameanza kujenga hoja
kuwa endapo hatadhibitiwa mapema, basi mambo yatakwenda mrama kwani
chama hicho kimekuwa kikinufaika na misaada kutoka kwa wafadhili
wanaokabiliwa na tuhuma za ukwepaji wa kodi.
Inahofiwa Rais Magufuli asipodhitibiwa mapema na chama, ipo siku
ataingilia makampuni yaliyoanzishwa na chama siku za nyuma na kuhusishwa
na ufisadi, kwa mfano Meremeta.
Inahofiwa kuwa rungu lake likifikia maeneo hayo, CCM itakuwa
imevuliwa nguo na kwamba hakuna kiongozi wa CCM atakayesalimika pale
atakapoanza kutumbua jipu la makampuni hayo na yale yaliyoanza kusaulika
mfano kashifa ya akaunti ya madeni ya nje (EPA).
Kwa msingi huo, vita vilivyoanza ndani ya chama hicho ni kutaka
kumfunda Rais Magufuli ili asichokonoe yaliyopita. Kwanza aanzie hapa
alikoishia mtangulizi wake. Asahau yaliyopita vinginevyo atatumbua
makovu ya majipu ambayo huenda hata yeye akashindwa kumpata daktari wa
kuyatibu.
Ninachotaka kusema ni kwamba kuna baadhi ya viongozi ndani ya CCM
ambao walihusika kwa njia moja au nyingine kutoa vibali na ‘vimemo’ kwa
wafanyabiashara wakubwa ambao wamekuwa wakivitumia kukwepa kulipa kodi
za serikali kwa maslahi binafsi. Hivyo kasi hii ya Rais itawaumbua
hadharani.
Kwa kutambua hali hiyo, vigogo hao wameanzisha ushirika bubu na
kambi ya upinzani ili kwa pamoja watafute mbinu za kuhujumu nguvu hizo
za Rais Magufuli. Wanadai eti hatafanikiwa bila ya kuungwa mkono na wana
CCM wenzake.
Vita vya pili vinahusu kambi ya upinzani. Mtoa taarifa alisema
kwamba, kambi ya upinzani nako hakuna usalama. Inaelezwa kuwa wapo
baadhi ya vigogo waliopo kambi hiyo ya upinzani ambao pia wana mahusiano
na wakwepa kodi.
Inasemekana baadhi ya viongozi kutoka kambi ya chama tawala
wanawapa nguvu wapinzani ili wamchefue Rais Magufuli kwa madai kwamba
anafanya kazi ya “One man show” yaani kazi bila ushirikiano na wenzake.
Kuna madai kuwa Rais Magufuli haambiliki, hashauriki, hasikii ya
mtu, hivyo anaweza kuleta madhara kwa taifa. Kauli mbiu yao ni kufuta
agenda ya mabadiliko na mbadala wake kuingiza agenda ya “katiba mpya” na
kutangazwa kwa matokeo ya Zanzibar.
"Jamaa atalazimika kujieleza kwenye kelele za wapinzani hivyo
agenda yake ya mabadiliko itakufa tu” alisema mtoa taarifa. Kimsingi
vita hivi vinataka kumtoa Rais Magufuli nje ya reli ili aachane na hoja
ya kutumbua majipu. Hata hivyo, wapiganaji wa vita hivyo wanaogopa nguvu
za Umma iliyopo nyuma. Tusubiri.
No comments:
Post a Comment