TTCL

EQUITY

Tuesday, December 2, 2014

Mvutano kuhusu mali ya Mandela waendelea

Bi Winnie Mandela alichana na hayati Mandela mwaka 1996
Serikali ya Afrika Kusini imepinga hatua ya kisheria aliyochukua aliyekuwa mke wa Nelson Mandelakutaka kupewa umiliki wa nyumba ya hayati Mandela katika mvutano unaoednelea kuhusu mali ya Mandela.
Katika ripoti ya korti,Bi Madikizela-Mandela alisema kuwa Rais wa kwanza mweusi wa Africa Kusini aliandikisha mali hiyo katika jina lake kinyume na sheria.
Mali ya Mandela ina thamani ya dola milioni 4.3
Mandela alimuoa Graca Machel mwaka 1998 alipokuwa anasherehekea miaka 80
Bi Mandela alitalakiwa na hayati mzee Mandela mwaka 1996 lakini alienda mahakamani kutaka mahakama kmpa haki ya kumiliki mali hiyo akisema kuambatana na utamaduni ana haki juu ya nyumba hiyo iliyo kijiji Qunu.
Bwana Mandela alifariki takriban mwaka mmoja uliopita bila ya kumtaja mkewe wa zamani kwa wasia wake.
Wawili hao walikuwa wanandoa mashuhuri sana wa kisiasa kwa miaka 38 hadi walipoachana.
Bwana Zuma aliungana na familia ya Mandela wakati wa mazishi ya hayati Mandela
Bwana Mandela alimuoa Bi Graca Machel mwaka wa 1998 alipokuwa akisheherekea miaka 80 tangu kuzaliwa
Kwenye ripoti iliyoko katika mahakama ya Mthatha, Bi Mandela alisema kuwa Bw Mandela alitumia sharia za ardhi vibaya kwa kujipa ardhi ya kibinafsi
Mawakili wake wanamtaka Rais Zuma na wizara ya maendeleo ya vijiji kutoa stakabadhi rasmi zinazoonyesha ardhi hiyo ni ilimilikiwa na Bwana Mandela
Nyumba ya Mandela inayong'ang'aniwa iko katika kijiji cha Qunu
Bi Madikizela-Mandela anaamini kuwa ardhi hiyo ni yake na alikabidhiwa na mfalme wa Aba Thembu Buyelekhaya Dalindyebo wakati Bwna Mandela alipokuwa gerezani. Anadai kuwa Mandela likwenda kinyume na sheria kujipa umiliki wa ardhi hiyo
Mzee Mandela alitoka jela mwaka 1990, miaka 27 baada ya kufungwa na kuchaguliwa kuwa Rais wa kwanza mafrika nchini humo mwaka 1994.

No comments:

Post a Comment