Kelele
ni moja ya mambo yanayosababisha uchafuzi wa mazingira.
Wakati mwingine
kelele husababisha mitetemo ambayo huleta bugudha kwa watu waishio au
walio jirani na eneo husika.
Nchi
nyingi duniani zimekuwa zikifanya jitihada kukabiliana na changamoto
mbalimbali za uchafuzi wa mazingira. Mikataba na itifaki mbalimbali
imesainiwa ili kuunganisha nguvu katika kukabiliana na changamoto hizo.
Kelele
ni moja ya mambo yanayosababisha uchafuzi wa mazingira. Wakati mwingine
kelele husababisha mitetemo ambayo huleta bugudha kwa watu waishio au
walio jirani na eneo husika.
Jiji
la Dar es Salaam linakumbwa na kadhia hii kutokana na shughuli
mbalimbali zinazofanyika. Magari ya matangazo yanapita mitaani huku
yakipiga muziki mzito bila kujali athari zake. Mengine husimama katika
maeneno yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na kufanya burudani wakati
wakitangaza bidhaa zao.
Baadhi
ya viwanda vimejengwa kwenye makazi ya watu. Mbali na kutoa moshi na
kutiririsha maji machafu, viwanda hivi vinatoa sauti na muungurumo
mkubwa ambao unasababisha adha kwa wakazi wa sehemu hiyo.
Madhehebu
ya kidini yanafanya mikutano yao ya injili na mihadhara katika maeneo
ya wazi na kupiga muziki kwa sauti ya juu. Nyumba nyingi za ibada
zimejengwa katikati ya makazi ya watu, jambo linalosababisha kero kwa
watu kwa kuwa baadhi yao hufanya shughuli zao kwa zaidi ya siku tatu za
wiki.
Mipango
miji mibaya inaelezwa kuwa chanzo cha kelele. Katika nchi nyingi
zinazoendelea watu wengi wanaishi kwenye nyumba ndogo na nyumba hizo pia
zimejengwa kiholela bila ya kuachiana nafasi. Hii inasababisha maeneo
hayo kuwa na mizozo na migogoro ya mara kwa mara.
Pia,
watu wengi sasa wanamiliki magari. Magari huongeza kiwango cha kelele
ambacho hakitakiwi. Makazi mengine yamejengwa karibu na viwanja vya
ndege, jambo linalowafanya wawe karibu na kelele kubwa za ndege wakati
zinapotua au kupaa.
Mkurugenzi
wa kampuni ya maendeleo ya makazi ya Space and Development, Renny Chiwa
anasema ujenzi holela hautakiwi kisheria na kuongeza kuwa Sheria ya
Mipangomiji ya mwaka 1956, na maboresho yake ya 1997 imepanga madaraja
ya matumizi ya ardhi ambayo kwa mfano, kuanzia A na B ni eneo la makazi,
K shule, N na M maeno ya viwanda ambayo hayachangamani na makazi.
“Makanisa,
misikiti, klabu za pombe ni taasisi ambazo hazitakiwi kuwa mbali sana
na makazi wala kuwa katikati ya makazi, bali zifikike kirahisi. Lakini
kwa sasa tunaona baadhi ya makanisa na klabu za pombe zikikimbilia
katika maeneo ya makazi na yasiyopimwa,” anasema Chiwa.
Mtaalamu
huyo anasema yapo maeneo ya biashara pekee na yale yenye mchanganyiko
na makazi. Lile lenye mchanganyiko wa makazi na biashara huwa na hoteli
zisizopiga muziki kwa sauti kubwa wakati eneo la biashara huwekwa
pembezoni mwa mtaa kwa ajili ya huduma na hapa ndipo masoko na vilabu
vya pombe hupatikana.
Sanjari
na kuongezeka kwa idadi ya taasisi zinazopiga muziki kwa kiasi kikubwa
na katikati ya maeneo ya makazi ya watu, mengine yakijengwa kinyume na
sheria, ipo pia burudani mpya maarufu kama vigodoro.
Vigodoro
vinazidi kuongezeka kila uchwao katika maeneo mengi ya ‘uswahilini’
ambapo wakazi wake hujikuta wakivumilia shida zitokanazo na furaha za
wengine ambao hukesha wakicheza ngoma na muziki usiku kucha.
Tayari jeshi la polisi lilishapiga marufuku, lakini bado vinaendelea kwa mitindo tofauti tofauti kutokana na hadhi ya eneo husika.
Tayari jeshi la polisi lilishapiga marufuku, lakini bado vinaendelea kwa mitindo tofauti tofauti kutokana na hadhi ya eneo husika.
Kama
hiyo haitoshi, baadhi ya wakazi wa jiji hili wenye sherehe zao
huzunguka mitaani na kuonyesha mbwembe za kuning’inia juu ya magari
yenye muziki mkubwa huku wakikata viuno.
Katika
utafiti wa kelele katika hoteli na migahawa mkoani Morogoro
uliochapishwa Desemba, 2009 katika jarida la Sayansi na Usimamizi wa
Mazingira (Jasem), Dafrozah Samagwa na wenzake wa Chuo Kikuu cha
Sokoine, walibaini kuwa asilimia kubwa ya hoteli zilikuwa zinapiga
muziki kwa kiwango kikubwa kati ya 61 dBA hadi 64dBA. dBA ni kipimo cha
kisayansi cha ukubwa wa sauti.
Kwa
mujibu wa utafiti huo ulioitwa Uchunguzi wa Upigaji Kelele katika
Migahawa ya Manispaa ya Morogoro, sauti zilizopimwa kutoka ndani ya
migahawa hiyo zilizidi kiwango kinachotakiwa na Shirika la Viwango
nchini (TBS) cha sauti isiyozidi 55dBA katika eneo lenye mchanganyiko na
makazi.
Pamoja
na vurugu zote hizo za kelele, bado mamlaka husika zinatajwa na baadhi
ya wadau kuwa hazijachukua hatua yoyote. Halmashauri ambazo hutoa leseni
za shughuli mbalimbali zinatuhumiwa kulegalega kiasi cha kuacha tatizo
liendelee.
“Hapa
tumezungukwa na makanisa matatu; moja kubwa na mengine madogo… yote
haya hupiga muziki kiasi cha kufanya mazingira haya kuwa magumu sana
kuishi,” anasema Dotto Magoma, mkazi wa Tabata Segerea.
“Wenzetu mitaa ya Kisukuru tumesikia waliokuwa wanapiga kelele wametimuliwa, lakini kwetu hali bado ngumu.”
Anasema
kuwa baada ya hali hiyo kuzidi na taasisi hizo kupiga muziki na
mapambio usiku kucha kuanzia Ijumaa hadi Jumapili, ilibidi wakazi wa
mtaa waombe kufanya kikao na balozi wao ili wajadili namna ya kuzungumza
na viongozi wa makanisa husika.
Athari za kelele kwa binadamu
Athari za kelele kwa binadamu
Jarida
la Oxford la Uingereza linaeleza kuwa kuishi kwa muda mrefu katika eneo
lenye kelele kufikia kiwango cha 85 – 90 dBA kunaweza kumfanya mtu kuwa
na usikivu hafifu au kuwa kiziwi kabisa.
Oxford
limefafanua kuwa kiwango hicho cha kelele kinaweza kusababisha magonjwa
mbalimbali ya moyo (cadiovascular) kama vile shinikizo la damu,
mfadhaiko wa moyo (hypertension) na msongo wa mawazo.
Pia,
imebainika kuwa kiwango kikubwa cha kelele kinasababisha kutopata
usingizi usiku. Inaelezwa kuwa kulala katika eneo lenye kelele
kunamfanya mtu asilale kwa muda mrefu, kuwa na hasira muda mwingi na
kuathiri ukuaji wa watoto.
Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa katika miji ya London na Los Angeles, kuna uhusiano mkubwa kati ya sauti kubwa zinazosababishwa na milio ya ndege na matatizo ya kisaikolojia na akili.
Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa katika miji ya London na Los Angeles, kuna uhusiano mkubwa kati ya sauti kubwa zinazosababishwa na milio ya ndege na matatizo ya kisaikolojia na akili.
Jarida
hili linafafanua kuwa baadhi ya watu wanakuwa na hasira, wengine kujawa
na hofu kulingana na aina ya kelele inayozalishwa. Linaeleza kuwa
matatizo yote haya ya kisaikoljia yanajitokeza kama mtu atakaa kwa muda
mrefu eneo lenye sauti zilizopitiliza kipimo.
Mamlaka zafafanua
Ofisa uhusiano wa manispaa ya Kinondoni, Sebastian Mhowela anasema sheria za kudhibiti kelele zipo katika ngazi ya halmashauri za manispaa, lakini utekelezaji wake unabaki kuwa katika ngazi ya serikali ya mtaa husika.
Ofisa uhusiano wa manispaa ya Kinondoni, Sebastian Mhowela anasema sheria za kudhibiti kelele zipo katika ngazi ya halmashauri za manispaa, lakini utekelezaji wake unabaki kuwa katika ngazi ya serikali ya mtaa husika.
Anasema
serikali ya mtaa au kijiji ina jukumu la kusimamia udhibiti wa kelele
ambazo zitaonekana kuwa kero miongoni mwa wanajamii.
Anafafanua
kuwa, kama mtu hajafurahishwa na kelele hizo anatakiwa kupeleka taarifa
serikali ya mtaa huo ili ichukue hatua stahiki.
“Hili
ni jambo dogo, tumekasimu madaraka kwa serikali za mitaa ili ziweze
kusimamia utekelezaji wake. Viongozi wa mitaa walione hili kama tatizo
na kuchukua hatua linapojitokeza,” alisema.
Hata hivyo, Mhowela anabainisha adhabu kwa kuvunja sheria hiyo ni faini ya Sh50,000.
Ofisa
huyo anasisitiza wananchi kutambua haki na wajibu wao kwa kuzifahamu
sheria ndogondogo zinazosimamiwa na halmashauri zao. Hatua hii inaweza
kuchukuliwa endapo mwananchi atashiriki kwa kutoa taarifa.
“Tatizo
hili tumelizungumzia sana, nadhani sasa wananchi watakuwa na utashi wa
kuchukua hatua. Si jambo la kutoa matangazo tu, pia yapo madhehebu
yanayoendesha mikutano yao katikati ya makazi ya watu kwa sauti ya juu
sana. Nao wanadhibitiwa kwa sheria hiyo hiyo,”
Anabainisha
kuwa manispaa pekee ndiyo hutoa vibali vya kufanya matangazo na katika
vibali hivyo wanapewa masharti ya kupiga kwa sauti ya kawaida.
Naye
ofisa habari wa Manispaa ya Ilala, Tabu Shaibu anasema ofisi yake
hufanya ukaguzi mara kwa mara na kwamba wale ambao hubainika,
huchukuliwa hatua za kisheria.
“Wakati wa kuomba na kupatiwa leseni kuna masharti kabisa mmliki wa klabu ya pombe au hoteli hutakiwa kuyafuata. Baadhi ya masharti hayo ni muda wa kufungua na kufunga pamoja na kiwango cha sauti ya muziki unaotakiwa,” anabainisha Shaibu.
“Wakati wa kuomba na kupatiwa leseni kuna masharti kabisa mmliki wa klabu ya pombe au hoteli hutakiwa kuyafuata. Baadhi ya masharti hayo ni muda wa kufungua na kufunga pamoja na kiwango cha sauti ya muziki unaotakiwa,” anabainisha Shaibu.
Mwishoni
mwa juma lililopita, mkurugenzi wa utekelezaji na uzingatiaji wa Nemc,
Dk Robert Ntakamulenga alinukuliwa na The Citizen, gazeti dada la
Mwananchi, akikiri kuwa ofisi yake inakosa sheria za kuwadhibiti wapiga
kelele licha ya kuwepo malalamiko lukuki.
“Tunapokea
malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya hili na baadaye hutembelea
eneo husika na kuamuru kusitisha upigaji kelele uliopitiliza, hata hivyo
mbinu hii haijaweza kutokomeza tatizo,” anasema Dk Ntakamulenga.
Hivyo,
udhibiti wa kelele katika maeneo ya makazi ni jukumu la wananchi kwa
kushirikiana na Serikali za mitaa. Wananchi washiriki kwa kutoa taarifa
pale wanapokumbana na adha hizo na Serikali za mitaa zisimamie sheria
zilizopo.
No comments:
Post a Comment