TTCL

EQUITY

Friday, July 5, 2013

WATANZANIA WATAKIWA KULIPIA SIM CARD

Maneno ya Mh. Zitto Kabwe kuhusu kodi mpya ya Tshs. 1,000/= kwa mwezi kwa kila laini ya simu

Maneno haya yameandikwa na Mh. Zitto Kabwe, jana tarehe 4 Julai kupitia akaunti yake ya Facebook:
“Kodi ya Tshs 1,000 kwa mwezi Kwa kila kadi ya simu uliyonayo imeanza rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi hii. Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na Wewe mwenye simu. Kampuni ya simu inakusanya Kwa niaba ya serikali. Ingawa sikuwepo wakati kodi hii inapitishwa na Bunge siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kuwa sehemu ya Bunge hili. Ni aibu Kwa kuwa pendekezo la kodi hii liliondolewa na Waziri wa Fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya Serikali. Pendekezo lilirudishwa namna gani kupitia muswada wa fedha, finance bill, Haieleweki. Ni skandali. Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye Bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu zaidi kwamba hatukupiga kelele za kutosha kuzuia jambo hili.”

No comments:

Post a Comment