TTCL

EQUITY

Thursday, June 27, 2013

CHADEMA HATUCHUKUI MILIONI 100 ZA SERIKALI KWA USHAHIDI WA ARUSHA


John Mnyika (MP)
Na Mwanablog

Pamoja na kuwa wana ushahidi wa Picha, Mikanda ya Video inayoonyesha jinsi Polisi walivyoshiriki kulipua bomu la Arusha, Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wamesema hawapo tayari kupokea pesa zilizotengwa na serikali kwa ajili ya mtu atakayetoa taarifa kuhusu waliohusika na mlipuko wa Arusha.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisi za Chama hicho Makao Makuu, Msemaji wa Chama hicho John Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo alisema “hata kama bado hatujakaa kama Chama kuafikiana suala hili, hizo pesa kuzichukua ni ufisadi tu, matumizi mabaya ya pesa, serikali imepata wapi pesa za kulipa milioni mia kwa watoa taarifa wakati haijawahi hata kutoa rambirambi kwa mjane wa Daudi Mwangosi, licha ya kwamba Polisi walihusika kwa asilimia zote katika kuua, hatuwezi kuhuchukua hizo pesa.

Kwanza ifahamike kwamba serikali imeamua kutenga hilo fungu ili kuhalalisha matumi mabovu ili kuhalalisha ulaji wa pesa, ije iseme tuliwalipa watoa taarifa, huu ni uongo, na serikali inapokuwa inadanganya raia wake inakosa uadilifu wa kuendelea kutawala. 

Suala la Arusha ni tete, serikali imekuwa ikisema uongo hapa na pale, ndio maana hata Mizengo Pinda tangu aseme uongo suala hilo halijawahi kuzungumzwa Bungeni, Spika analipiga danadana kila mara.

Aidha katika mkutano huo, Mnyika amelitaka jeshi la polisi liwaachie vijana watatu wanaoteswa na Jeshi hilo ili kuwalazimisha kutoa mikanda waliyorekodi ambayo Mbowe anasema wanayo inayoonyesha jinsi Polisi walivyolipua bomu, kuwapiga risasi watu waliotaka kumkamata aliyelipua bomu, na gari ya polisi iliyomtorosha mtu aliyerusha bomu. Jeshi la Polisi mkoani Arusha linawashikilia vijana watatu makada wa Chadema, ili liweze kupata mikanda hiyo kwa nguvu bila kutumia njia za kuwaomba.

No comments:

Post a Comment