TTCL

EQUITY

Monday, April 25, 2016

Uanzishwaji maeneo ya kiutawala ni mgumu-TAMISEMI

Serikali imesema kuwa uanzishwaji wa maeneo mapya ya utawala kwa ajili ya kupelekea huduma muhimu wananchi karibu zaidi ni suala gumu kiutekelezaji ambalo linahitaji uvumilivu kutoka kwa wabunge wanaomba uundwaji huo kutokana na ufinyu wa bajeti.
Waziri wa TAMISEMI, Mhe George Simbachawene.
Akitolea ufafanuzi juu ya suala hilo leo Bungeni,Waziri wa TAMISEMI,Mhe George Simbachawene, amesema kuwa kuna maombi mengi kutoka kwa wabunge ambao wanataka maeneo yao kuanzishwa kwa halmashauri au wilaya suala ambalo ni gumu kutekelezeka kutokana na bajeti ya serikali.

Mhe. Simbachawene amesema kuwa wabunge wengi wameahidi wananchi wao kuwa watayafanya maeneo yao kuwa na halmashauri au Miji midogo hali ambayo inakua vigumu kwa serikali kujenga ofisi kuu za maeneo hayo mapya kwa wakati wanahitaji wabunge.

Mhe. Simbachawene amewataka wabunge hao kuwa wavumilivu wakati serikali ikiendelea kuongeza bajeti ya kuboresha maeneo mapya yaliyoanzishwa lakini pia wanaendelea kufuatilia mchakatao wa uanzishwaji wa maeneo hayo.

No comments:

Post a Comment