Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amehitimisha ziara yake ya siku tatu mkoani Ruvuma kwa kuzungumza na waandishi wa habari.
Katika majumuisho ya ziara yake aliyoyafanya kwenye ukumbi wa
mikutano wa Ikulu Ndogo ya Songea, Majaliwa alielezea kuridhishwa kwake
na miradi aliyoikagua.
Mbali na kuridhishwa huko, aliwaagiza watendaji wa serikal katika
ngazi za halmashauri kuhakikisha tatizo la madawati kwenye shule za
msingi na sekondari, linapatiwa ufumbuzi kwa kutumia vyanzo vya ndani.
Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri kushirikiana na viongozi wa
serikali kuu kutatua tatizo hilo kwa kutumia mbao zinazokamatwa baada ya
kuvunwa bila kufuata taratibu, badala ya kuzitunza kwa kuzilundika tu.
Kuhusu uchimbaji wa makaa ya mawe unaofanywa katika kijiji cha
Ngaka wilayani Mbinga na kampuni ya TANCOAL, Waziri Mkuu alisema
serikali inafanya mapitio ya mkataba wa makubaliano kuhusu huduma za
jamii.
Waziri Mkuu alisema kupitia Wizara ya Nishati na Madini, pia
mikataba yote ya kampuni za uchimbaji madini zilizoko nchini ambazo
zimeanza kupata masoko ndani na nje ya nchi, itapitiwa upya.
Alisema hivi sasa kuna viwanda vingi vinavyotumia makaa ya mawe,
hivyo serikali kupitia wizara yenye dhamana ya madini, itapitia upya
mikataba yote ili kuona makubaliano yaliyomo kuhusu huduma za jamii
zinazopaswa kutolewa na kampuni hizo.
Kwa mujibu wa Majaliwa, lengo la kufanya hivyo ni kuondoa
malalamiko ya muda mrefu, ambayo yamekuwa yakitolewa na wananchi
wanaoishi kwenye maeneo yanayozunguka migodi mbalimbali nchini.
No comments:
Post a Comment