Serikali imesema kuwa Licha ya juhudi za wadau wa
 kimataifa na serikali, ugonjwa wa kipindupindu bado umeendelea kuuwa 
watu wengi nchini Tanzania huku changamoto kubwa ikibainishwa kuwa watu 
kutozingatia usafi wa mazingira na kanuni za Afya.
Mtaalamu wa afya ya jamii ya epodemiolojia Dk Azma Simba kutoka 
wizara ya afya (Mwenye t-shirt Nyeusi) akiwaeleza jambo wataalam wa Afya
 kutoka nje
Akizungumza
 kwa njia ya Simu na East Africa radio mtaalamu wa afya ya jamii ya 
epodemiolojia Dk Azma Simba kutoka wizara ya afya amesema kuwa  licha ya
 kwamba kwa baadhi ya mikoa mlipuko wa kipindupindu unadhibitiwa lakini 
kwa ujumla ugonjwa unasambaa kwa kasi ambapo zaidi ya watu 12,000 
wameripotiwa kuathirika na Ugonjwa huo.
Dkt. Simba amesema kuwa kile anachokiona kinakwamisha kutokomeza kwa kasi kipindipindu Tanzania ni kukosekana kwa ushirikiano toka kwa jamii katika kuitikia wimto wa utunzanji wa mazingira pamoja na kuzingatia kanuni za afya.
Takribani watu 200 wamefariki dunia kutokana na mlipuko wa kipindupindu nchini Tanzania ambao ulianza mnamo Agosti 15, 2015.
Dkt. Simba amesema kuwa kile anachokiona kinakwamisha kutokomeza kwa kasi kipindipindu Tanzania ni kukosekana kwa ushirikiano toka kwa jamii katika kuitikia wimto wa utunzanji wa mazingira pamoja na kuzingatia kanuni za afya.
Takribani watu 200 wamefariki dunia kutokana na mlipuko wa kipindupindu nchini Tanzania ambao ulianza mnamo Agosti 15, 2015.
No comments:
Post a Comment