Leo ni siku ya tatu, kwenye siasa
Tanzania kuna story kubwa ambayo bado inaendelea kuchukua Headlines
kubwa, ni ishu ya Uongozi wa CHADEMA kutangaza kumsimamisha Uanachama
Mbunge Zitto Kabwe.
Jana na leo Magazetini na kwenye vyombo
vya habari kuna taarifa ya kingine alichokisema Mbunge huyo kuhusu
taarifa za kusimamishwa uanachama; “Mimi
ninaendelea na kazi kama hakuna kilichotokea.. Sina taarifa rasmi ya
chochote ambacho kimetokea ndio maana ninaendelea na kazi.. Maamuzi
yoyote ambayo yanatokea ni process. Hata ikiwa kwa mfano maamuzi ya
chama ni kama ilivyotangazwa kuna process ya kuandika barua kwa Spika..
Spika kujiridhisha..
Minutes
za vikao kwa sababu maamuzi yote ni lazima yafanywe na vikao sio mtu
mmoja.. then Spika ananiandikia mimi… Kama nyinyi mnavyosikia kwenye
vyombo vya habari na mimi hivyi hivyo nasikia… siwezi kujibizana na
Chama changu“– Zitto Kabwe.
No comments:
Post a Comment