TTCL

EQUITY

Monday, March 16, 2015

ZITTO KABWE ATANGAZA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE..

Baada ya kutemwa na CHADEMA, Zitto Kabwe ameenda jimboni kwake Kigoma Kaskazini kuzungumza na wananchi wake. 

Pichani ndiyo mapokezi aliyopata huko jimboni, watu wengi wamejitokeza kumpokea na kelele zikisikika ..ZITOO...ZITOOO..ZITOOO...
Zitto Kabwe hivi punde katika ukurasa wake wa Twitter na Facebook ameandika maneno yafuatayo


"Leo nimekutana na wazee wa jimbo la kigoma kaskazini na wawakilishi wa vijiji vyote 45, nimewaaga rasmi kuwa sitagombea ubunge jimbo hilo"

Ujumbe mwingine alioandika huu hapa

"Nimewashukuru kwa kunipa fursa kutoa utumishi wangu kwao kwa miaka 10. Kwa niaba yao wote Mzee Mahmoud Bikulako alifanya dua na maombi rasmi"

Mwingine huu hapa

 "Wazee wamenibariki kuchukua maamuzi yanayofaa kulingana na hali ya kisiasa inayoendelea hivi sasa"

"Kisheria, kikatiba, kikanuni Mimi bado ni mwanachama wa chama nilichotumia kuingia bungeni mwaka 2010"

4mwndg
Wakazi wa Kigoma Kaskazini  jana walikusanyika pamoja kumsikiliza Mbunge wao Zitto Kabwe ambaye siku ya jana ameamua kuitumia rasmi kama kuwaaga wananchi  na wapiga kura wa jimbo lake.
Zitto Kabwe ambaye ijumaa ya wiki hii kupitia mtandao wa kijamii kwenye akaunti yake ya Twitter ali break news kwamba hatogombea tena Ubunge kwenye uchaguzi ujao wa mwishoni mwa mwaka huu.
1mwndg
6mwndg
5mwndg
2mwndg

No comments:

Post a Comment