TTCL

EQUITY

Thursday, April 3, 2014

Magonjwa yasiyoambukiza huua Watu Milioni 8 kila mwaka!


TANZANIA inatajwa kuwa miongozi mwa Nchi zinazoendelea, kuwa na Idadi kubwa ya Watu wanaosumbuliwa na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, ambapo zaidi ya Watu (milioni Nane) hufariki kila mwaka kutokana na Magonjwa hayo.

Takwimu za Kidunia pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO) za mwaka 2012/2013, zinaonyesha kuwa karibu Watu milioni 35 hufariki ndani ya mwaka mmoja, hali ambayo inachangaia kushuka kwa Uchumi.
Katika mpangowa upimaji wa Afya kwa magonjwa yasiyoambukiza Jijini Dar es salaam, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umebaini kuwa Idadi kubwa ya Wanaume wanapatwa na magonjwa hayo kuliko Wanawake.

Uchambuzi huo umeonyesha magonjwa yasiyoambukiza Kama, Kisukari, Shinikizo la damu, na Saratani zote ambazo zimekuwa chanzo cha Vifo hivyo, huku Serikali ikisema imeamua kuongeza juhudi za makusudi kupambana nayo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mfuko wa bima ya Afya, athari ya magonjwa yasiyoambukiza ni mara (Nne) zaidi ya watu waliopo mijini kuliko vijijini, huku asilimia 12.8 ya wanaougua wakiwa wako mijini na aslimia 3.1 wako vijijini kutokana na mfumo wa maisha.

No comments:

Post a Comment