TTCL

EQUITY

Monday, November 18, 2013

MAZOEZI NA AFYA ZETU


Mwili wa binadamu waweza pia kufananishwa na nyumba kwasababu nyumba ili ikamilike inahitaji uuwepo wa matofali,mchanga, simenti na malighafi nyingine nyingi na inahitaji ukarabati wa mara kwa mara ili iweze kuwa nyumba bora.

Watu husema kuwa mwili haujengwi na matofali bali kwa vyakula vitatakavyo uwezesha mwili katika utendaji wa kazi mbali mbali lakini pia mazoezi ya viungo ili kufanya mwili kuwa imara zaidi na wenye nguvu. Mwili wa binadamu unapokosa mazoezi ya kutosha hufanya mwili kunyong’onyea na fufanya baadhi maeneo katika mwili kushindwa kufanya kazi vizuri kama inavyotakiwa.
Mazoezi ya mara kwa mara au kufanya kazi zinazohusisha matumizi ya nguvu ya mwili yanasaidia mifumo mingi ya mwili kufanya kazi inavyotakiwa, mazoezi yatatuepusha na magonjwa ya moyo, kisukari, na hata magonjwa mengine hayataweza kushambulia miili yetu, na ni njia nzuri ya kupunguza uzito wa mwili uliozidi. Unapokuwa unafanya mazoezi mara mara utafaidika na mambo yafuatayo:
Mwanamke akifanya mazoezi ya viungo.
Moja ni kuongeza nafasi ya kuboresha umri wa kuishi na kuishi katika afya njema.
Pili mazoezi yanasaidia kutulinda na kutuepusha na magonjwa nyemelezi kama homa na magonjwa ya moyo na magonjwa yanayoambatana nayo kama shinikizo la damu na ongezeko au kiwango cha juu cha damu katika mwili. Kiwango cha juu cha damu katika mwili kimekuwa kisababishi cha ongezeko la shinikizo la damu na hata kuwa katika hatari ya kupata kiharusi.
Tatu mazoezi yanatusaidia kuepukana na magonjwa ya kansa  kama kansa ya tumbo, kansa ya matiti, kansa ya mapafu na kansa ya kizazi. Hii ni kwa sababu mazoezi yanaboresha mifumo mbali mbali ya mwili na kuwezesha mwili kutoa taka na sumu mbali mbali mwilini, pamoja na kuimarika kwa kinga ya asili ya mwili.
Nne mazoezi husaidia kuongeza uwezo wa kuona mbali hasa kwa wazee na watu watu wa makamo lakini kwa sasa tatizo hili linawakumba mpaka vijana kwa sababu vijana wengi hawafanyi mazoezi
Pia mazoezi yanasaidia kutukinga na kisukari aina ya pili (ugonjwa ambao mtu anaupata ameshakuwa mkubwa na sio kwa kuzaliwa), na kutukinga na matatizo ya mmeng’enyo ambayo yanaweza kutuletea magonjwa ya moyo na kisukari pia.
Mazoezi husaidia kuimarisha afya ya akili, yanasaidia kutuepusha na magonjwa ya kupoteza kumbukumbu hasa kwa wazee. Pia mazoezi yanatuondolea msongo wa mawazo, woga na mtu kuwa katika afya nzuri ya akili.
Mazoezi yanasaidia kuwa na mapafu yenye kufanya kazi vizuri,moyo wenye afya na kuimarisha misuli ya mwili kwa ujumla. Bila kusahau kuwa mazoezi husaidia kupata usingizi mzuri kwa afya bora.

Mazoezi ni sehemu muhimu ya kuzingatia katika kuujenga na kuulinda mwili wako ili usikumbwe na magonjwa na matatizo yatakayo ufanya mwili kudhoofu katika utendaji wa kazi mbali mbali katika mwili.

No comments:

Post a Comment