TTCL

EQUITY

Saturday, August 17, 2013

HUYU NDIYE SHILOLE "ZENA MOHAMMED YUSUPH"


KUKUA kwa tasnia ya filamu Tanzania kunakwenda sambamba na kuibuka kwa vipaji vipya vya waigizaji mahiri na wenye mvuto kila kukikcha.

Mmoja kati ya Zena Mohamed Yussuf maarufu kama ‘Shilole’ ambaye tangu ajikite katika tasnia hiyo ameweza kuonyesha uwezo na kiwango cha hali ya juu licha ya kuwa amecheza filamu nne ambazo zimeshatoka mpaka sasa .
Kwa wanaofuatilia filamu hizo watakumbuka jinsi alivyofanya kweli katika ‘Fair Desecion’ akicheza na Ray, Johari na wengineo,ikifuatiwa ‘Crazy Of Love’ aliyocheza na Basupa, David Mjata na wengineo, ‘Pigo’ aliyocheza na Cloud na Aunty Ezekieli kabla ya kuibukia katika ‘Bed Rest’ akicheza na Ray, Thea, Johari na Mainda.

Hivi karibuni msani huyo ataonekana katika filamu mpya iliyosheheni nyota kibao katika nyanja mbalimbali nchini ‘Cut Off’ ambayo ipo katika matayarisho ya mwisho mwisho kabla ya kuingia sokoni.

Filamu hiyo kali na ya kusisimua mbali na Shilole pia imeigizwa na wakali wengine wakiwemo Rose Ndauka, Cloud, Cheki Budi, Aunty, Darleen na wengine.

Akizungumzia tasnia nzima ya sanaa ya filamu nchini anasema kwamba imeonekana kuvamiwa kutokana na baadhi ya watu kuamua kujikita baada ya kuoana wamekosa kazi ya kufanya,huku pia wakiwa hawana vipaji hali ambayo inafanya sanaa hiyo idharaurike na kuonekana ya wababaishaji.

“Kiukweli sanaa yetu inapanda lakini kuibuka kwa watu kibao kila mmoja akijifanya msanii wakati hana kipaji kunatutilia doa na kufanya tuonekane waigizaji wote ni wababaishaji”, Anasema.

Shilole, likiwa na maana ya kioo alilopewa na bibi yake anasema kabla ya kufikia hapo alipo alipitia milima na mabonde katika kazi yake kitu anachokiona kuwa ni changamoto katika maisha yake ambavyo pia anaamini vinasaidia katika kuboresha na kukuza kipaji alichonacho.

Pamoja na hilo anasema hakukata tamaa kwani amedhamiria kuhakikisha anakuwa msanii mwenye jina kubwa zaidi alilonalo nje ya Tanzania na mipango yake zaidi kucheza hadi Hollywood.

“Ninataka kuwa first lady wa bongo movie siku moja, hilo linawezekana kwani ni moja ya dhamira yangu katika medani hii”, Anasema Shilole ambaye kabla ya kufikia hapo aliwahi kupitia katika kikundi kilichokuwa chini ya mpiga gitaa wa kundi la Jahazi Modern Taarab, Thabit Abdul ‘Mtoto wa Ilala’.

Akizungumzia hali ya sanaa hiyo kwa sasa anasema imekuwa ikikuwa kwa kasi kwa pamoja na kuibuka kwa waigizaji wengi, hata kipato wanacholipwa kimepanda akitolea mfano yeye alianza kucheza kwa ujira mdogo wa sh.20,000 lakini kwa sasa analipwa mpaka sh. 300,000 na kuendelea kwa ajili ya kazi hiyo.

Anaongeza kuwa kuibuka huko kwa wasanii kumeleta ushindani huku akimtaja Aunty Ezekiel kama ni mwanadada mkali.

No comments:

Post a Comment