TTCL

EQUITY

Monday, February 27, 2017

Philip Bilden akataa kuchukua wadhifa baada ya kuteuliwa na Trump

media Philip Bilden, mteuliwa wa Rais Donald Trump akataa kuchukua wadhifa. REUTERS/Carlos Barria
Rais wa Marekani Donald Trump, amemteua Philip Bilden kujaza wadhfa wa waziri wa jeshi la wanamaji lakini muda mchache baadaye afisa huyo amekataa kuchukua wadhifa huo baada ya kuonekana kukiuka sheria za taifa kuhusu mgongano wa maslahi.
Philip Bilden ni mtu wa pili kuteuliwa na Rais Trump na kukataa kuchukua wadhifa. Mapema Mwezi huu mteuliwa wa Rais Trump aliyependekezwa kusimamia jeshi la Marekani alijiondoa kwenye wadhifa huo.
Philip Bilden ameeleza wasiwasi wake kuhusu maisha yake ya usiri na changamoto alizokumbana nazo katika kujitenganisha na biashara zake.
Hata hivyo Waziri wa usalama, Jim Mattis, amesema atampendekeza mtu atakayechukua nafasi ya Bilden katika kipindi cha siku chache zijazo.
Rais Donald Trump ameendelea kukukabiliwa na hali ya sintofahamu na kukosolewa ndani na nje ya nchi ya Marekani kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya wahamiaji hasa raia wa kigeni waishio nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment