TTCL

EQUITY

Thursday, June 2, 2016

“Shida za wanafunzi wa UDSM nazijua na nimeziishi” – Rais Magufuli

 
Siku moja baada ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kugoma kwa kukosa mikopo ya kuwakimu kimaisha, Rais Dk. John Pombe Magufuli amewambia wanafunzi wa chuo hicho kuwa anaelewa changamoto zinzowakabili wanafunzi hao.
Dk. Magufuli alisema hayo wakati alipokuwa akifanya uzinduzi wa jiwe la msingi la ujenzi wa maktaba ya kisasa ambayo itajengwa chuoni hapo kwa udhamini wa serikali ya China wenye thamani wa Dola Milioni 41.2.
Rais Magufuli alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imejipanga kuyafanyia  kazi matatizo yaliyopo chuoni hapo na kuwaahidi wanafunzi wa chuo hicho kikubwa nchini kuwa hatawaangusha atahakikisha matatizo yaliyopo chuoni hapo yanatafutiwa usumbufu.
“Chuo hiki kina historia kubwa Afrika na hata duniani, shida ambazo zinawapata wanafunzi wa UDSM hata mimi nimeziishi niwambie tu jambo moja kuwa sitawaangusha,” alisema Dk. Magufuli.
Aidha Rais Magufuli ameimwagia sifa serikali ya China kwa ufadhili huo nakuitaja kama moja ya nchi iliyo na urafiki wa kweli na Tanzania lakini pia kumpongeza Rais wa awamu ya nne na Mkuu wa Chuo cha UDSM, Dk. Jakaya Kikwete kwa kuomba ufadhili huo akiwa madarakani na sasa matokeo yake yanaonekana kuwa mazuri.
Kwa upande wa Mkuu wa Chuo hicho ambaye ni Rais wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete alisema chuo hicho kina changamoto nyingi zikiwepo miondombinu na upatikanaji wa maji safi na hivyo kumuomba Rais Magufuli kuangalia jinsi anavyoweza kumaliza changamoto hiyo.
“Wakati sisi tunaingia tulikuwa 350 ila kwa sasa wanafika hadi 7,000 kwa mwaka kwahiyo nikuombe uangalie ni jinsi gani utatusaidia kumaliza changamoto hizi, ulinipa kazi na mimi nimeifanya kama ulivyoniagiza,
“Changamoto ni nyingi na hata ukiangalia asilimia 30 pekee ya wanafunzi wa chuo ndiyo wanapata nafasi katika hosteli za chuo wengine asilimia 70 wanajua wenyewe wanapoishi na kama unavyofahamu wengi wanatoka maeneo ya mbali inakuwa ni changamoto kubwa kwao,” alisema Dk. Kikwete.

No comments:

Post a Comment