Makocha wazawa nchini wametakiwa kuzingatia
weledi wa kazi yao kwa umakini mkubwa ili kuongeza ushindani kwa makocha
wa kigeni wanaoonekana kuwa ndio bora zaidi yao kwenye klabu mbalimbali
hapa nchini.
Mkufunzi wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF katika picha .
Akizungumza
na East Africa Radio mkufunzi wa shirikisho la soka barani Afrika CAF
Wilfred Kidau amesema haoni utofauti wa makocha wazawa na wale wa kigeni
ambao wanaonekana kupewa kipaumbele na viongozi wa klabu nyingi hapa
Tanzania.
Kidau ameongeza kuwa tatizo kubwa ni makocha wengi wazawa wanakosa
mafunzo mengi ya vitendo ambayo yangewasaidia kujua kile wanachojifunza
kwa nadharia darasani na namna ya kukifundisha viwanjani.
Aidha mkufunzi huyo amewataka makocha kujitahidi kwa hali na mali
kujiamini na kuonesha wana uwezo kama ilivyo kwa Mecky Mexime ambaye
anaonesha ubora wake na klabu ya Mtibwa Sugar inayoshiriki ligi kuu ya
soka Tanzania bara.
Pia Kocha wa siku nyingi na mchambuzi wa mpira wa
soka nchini Tanzania Kenny Mwaisabula "Mzazi" amesema klabu ya Simba
haipo makini katika kuchagua makocha sahihi na ndio maana inatimua
makocha kila wakati.
Kocha
wa siku nyingi na mchambuzi wa soka nchini Tanzania Kenny Mwaisabula
"Mzazi" amesema klabu ya Simba haipo makini katika kuchagua makocha
sahihi na ndiyo maana inatimua makocha kila wakati.
Mwaisabula amesema ni kitu cha kushangaza kwa Simba kumfuta kazi Dylan Kerr wakati hadi sasa ameifikisha Simba nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara.
Mwaisabula ambaye aliwahi kuifundisha klabu ya soka ya Yanga, amesema Simba kuna tatizo la maamuzi ya kutafuta makocha, hivyo baadhi yao wanageukana pale mambo yanapoharibika na akaitaka ikae chini na kufikiria wapi wanakosea.
Uongozi wa Simba umeachana na kocha huyo baada ya miezi 6 ya mkataba wa mwaka mmoja na kuvunja huko mkataba ni makubaliano ya pande mbili.
Mwaisabula amesema ni kitu cha kushangaza kwa Simba kumfuta kazi Dylan Kerr wakati hadi sasa ameifikisha Simba nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara.
Mwaisabula ambaye aliwahi kuifundisha klabu ya soka ya Yanga, amesema Simba kuna tatizo la maamuzi ya kutafuta makocha, hivyo baadhi yao wanageukana pale mambo yanapoharibika na akaitaka ikae chini na kufikiria wapi wanakosea.
Uongozi wa Simba umeachana na kocha huyo baada ya miezi 6 ya mkataba wa mwaka mmoja na kuvunja huko mkataba ni makubaliano ya pande mbili.
No comments:
Post a Comment