Tiffah wa Dimond.
WATOTO wamekuwa wakileta furaha kwa walio wengi, wawe walio kwenye ndoa au hata wale ambao wako kwenye uhusiano wa kawaida.
Hali hiyo imesababisha kila
anayebahatika kuitwa mama au baba kutumia nguvu kubwa kuufahamisha
ulimwengu kuwa na yeye ana uwezo wa kuzaa.
Mtoto wa Kiba.
Katika hili wapo mastaa ambao
wanapojaaliwa kuwa na watoto, hutumia muda wao mwingi kuwatangaza kwenye
mitandao ya kijamii kila wakati. Mastaa wengi, kama ni mwanamke
akijifungua lazima ataanza vurugu mtandaoni, ataposti kampakata, mara
anamlisha. Yaani ilimradi kuonesha tu furaha aliyonayo.
Maleeka wa Mwana FA.
Kama ni mwanaume, mpenzi wake au mkewe
akijifungua, kila wakati atapiga picha za mapozi na kuzitupia mtandaoni.
Hii yote ni kuwarusha roho wenzao sambamba na kuonesha ni jinsi gani
watoto hao wamewaongezea furaha katika uhusiano wao.
Paula wa Kajala.
Wiki hii katika makala haya
nimekuandalia watoto 10 wa mastaa wa Bongo ambao picha zao hazikauki
mtandaoni. Katika hao, wapo waliofunguliwa na wazazi wao kurasa kwenye
Instagram na Facebook kama vile mtoto wa Diamond, Tiffah, Tanzanite na
Patrick.
Tanzanite wa Hbaba.
Mbali na hilo, wapo ambao wanawaandaa
watoto wao kuwa mastaa wa kesho kwa kuwasukumizia kwenye fani f’lani
mapema kabisa. Kwa mfano, mtoto wa H. Baba anaonekana kupendelea
uigizaji na muziki.
Patrick wa Muna.
Patrick wa Muna naye ni muigizaji mzuri tu.
Tiffah, baba yake aliwahi kusema
anapenda aje kuwa mwanamuziki. Yule wa Chuchu Hans ni muigizaji mzuri na
Paula wa Kajala anaelekea kwenye uanamitindo.
No comments:
Post a Comment