Baadhi ya shule za msingi katika Manispaa ya
Mtwara Mikindani zimeonyesha wasiwasi wao juu ya kasi ya wanafunzi
wanaojiandikisha na darasa la kwanza kuwa kubwa na kuhofia kuzidi idadi
inayokidhi mahitaji ya shule, kwa hofu ya wanafunzi kukosa kwa ku
Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, Donald Nssoko.
Wakizungumza
na East Africa Radio kwa nyakati tofauti, walimu wa kuu wa shule za
Kambarage na Ligula mjini humo wamesema kutokana na waraka wa elimu
uliowafikia katika shule zao kuwataka wasiwakatae wanafunzi,
watalazimika kuwapokea hata kama watafikia idadi inayokidhi mahitaji ya
shule.
Kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Mtwara Mikindani, Donald Nssoko,
amesema licha ya changamoto hizo, walimu wanatakiwa kuendelea kuwapokea
wanafunzi kama maagizo yanavyosema na kwamba kama kuna changamoto zozote
wanatakiwa kuwasiliana na uongozi wa manispaa.
Aidha, baadhi ya wazazi walioambatana na watoto wao kwa ajili ya
kwenda kuwaandikisha elimu ya msingi, wameelezea furaha yao juu ya
mpango wa elimu bure na kusema umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza
majukumu ya mzazi kwa mwanafunzi, huku wakikiri kuto takiwa kuchangia
kitu chochote zaidi ya kutekeleza wajibu wao wa kuwaandaa watoto kwa
yunifomu, daftari na kalamu.
No comments:
Post a Comment