TTCL

EQUITY

Friday, January 29, 2016

MBWANA SAMATTA ATUA UBELGIJI KUKAMILISHA USAJILI

Samatta-JPN 6
Taarifa kutoka nchini Ubelgiji zinasema kwamba, mchezaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga kwenye klabu ya TP Mazembe ya nchini Congo DR Mbwana Samatta muda wowote anaweza kujiunga na klabu ya Genk inayoshiriki ligi kuu nchini Ubelgiji (Belgian Pro League).
Kwa muda mrefu sana kulikuwa na harakati za Mbwana Samatta kujiunga na vilabu vya Ulaya, klabu ya Genk ya Ubelgiji kwa asilimia nyingi ipo kwenye dakika za mwisho kukamilisha deal la kumsajili Mbwana Samatta kutoka TP Mazembe.
Genk ipo nafasi ya sita (6) kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka nchini Ubelgiji ikiwa imecheza michezo 20 na kufanikiwa kukusanya jumla ya pointi 28 hadi sasa.
Moise Katumbi ambaye alikuwa anaonekana kama kikwazo yupo Ubelgiji na jana alikuwa anafanya mazungumzo na timu ya Genk na kufikia makubaliano ambapo na yeye pia amekubali kumruhusu Mbwana Samatta.
Dirisha dogo la usajili kwa vilabu vya Ulaya litakapofunguliwa mwezi January Samatta atatua Belgium kujiunga na klabu hiyo.
Samatta amebakiza mkataba wa miezi minne pekee kuendelea kusalia kwenye klabu yake ya TP Mazembe ambayo msimu huu ameisaidia kutwaa kombe la klabu bingwa Afrika.

Samatta akizungumza kwa mara ya kwanza na waandishi wa habari kwenye press conference tangu ajiunge na klabu ya Genk
Samatta akizungumza kwa mara ya kwanza na waandishi wa habari kwenye
press conference tangu ajiunge na klabu ya Genk
Mara baada ya Mbwana Samatta kukamilisha taratibu zote za kujiunga na klabu ya Genk, nyota huyo wa kwanza kutoka Bongo kwenda kucheza professional soccer barani Ulaya aliongea mbele ya waandishi wa habari akieleza anavyojisikia mara baada ya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na klabu hiyo.
Samatta amesema alikuwa anahisi anakuwa chizi kutokana na furaha aliyokuwa nayo baada ya dili hilo kukamilika ambalo limeifanya ndoto yake ya siku nyingi ya kucheza soka la kulipwa barani Ulaya kukamilika.
“Nilikuwa nahisi nakuwa chizi kutokana na furaha niliyokuwa nayo. Ukiwa na ndoto halafu unaona ndoto yako inakuwa kweli, na kilichotokea ni kama kuna giza mbele na unashindwa kuona hicho ndicho kilichotokea kwangu”, alisema Samatta.
“Naiheshimu TP Mazembe, namuheshimu Rais wa Mazembe Moise Katumbi. Sitaki kusababisha matatizo yoyote na wao kwasababu wamenichukua tangu nikiwa mdogo na kunilea. Nimekulia Mazembe nikisubiri wakati muafaka hadi klabu yangu ifikie makubaliano na klabu inayonihitaji”.
Samatta amesaini kandarasi ya miaka minne (4) kukitumikia kikosi cha Genk ambapo anatarajia kuhudumu kwenye klabu hiyo hadi mwaka 2020.

No comments:

Post a Comment