TTCL

EQUITY

Wednesday, December 2, 2015

TRA Mwanza washindwa kufikia lengo

Taswira ya jiji la Mwanza
Taswira ya jiji la Mwanza

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Mwanza imeshindwa kufikia lengo la ukusanyaji wa mapato katika kipindi cha mwaka 2013 – 2014, bila kubainishwa sababu za msingi zinazochangia ukusanyaji mdogo wa mapato.
Hayo yaliibuka jana wakati wa ziara ya Mkuu huyo, alipozungumza na wafanyakazi wa TRA namna ambavyo wanaendesha shughuli zao za ukusanyaji wa mapato pamoja na changamoto zinazowakabili.
Meneja wa TRA Mkoa wa Mwanza, Elinsa Nyange, amesema TRA ilikusudia kukusanya Sh. 4. 99 trilioni, katika kipindi cha mwaka 2013 lakini ilikusanya Sh. 123 bilioni.
Pia amesema katika kipindi cha mwaka 2014, TRA ambayo inakusanya kodi mikoa ya Mwanza na Geita iliweka lengo la kukusanya Sh 7.69 trilioni lakini ilikusanya Sh. 123 bilioni, huku akishindwa kubainisha sababu za msingi zinazosababisha kushindwa kukusanya kodi.
“Rais wa mkoa (Mkuu wa Mkoa wa Mwanza) nakuhakikishia tutaendelea kuwaelimisha wananchi juu ya umhimu wa ukusanyaji wa kodi, pia mkoa wetu na mikoa kama Arusha hailingani kwa vitega uchumi,” amesema Nyange.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo amesema sababu zinazotolewa na meneja huyo hazina tija kwani ukusanyaji wa mapato kwa mkoa wa Arusha upo juu ikilinganishwa na Mwanza.
Mulongo amesema kuwa mkoa wa Arusha katika kipindi cha mwaka 2013 ilikusanya Sh. 1.27 trilioni ikilinganishwa na Mwanza na Geita ambayo inakusanya Sh. 123 bilion kitendo ambacho ni aibu kwa mikoa hiyo.
Hata hivyo amesema licha ya mkoa Mwanza kuwa ni moja kati ya mikoa nchini yenye kiwango kikubwa cha uchumi ambao alidai unafikia trilioni 9, ukusanyaji wa mapato hafifu unachangiwa na watendaji wabovu.
“Serikali ya awamu ya tano inahitaji fedha na fedha zenyewe zinatoka kwenu na inafahamu pesa zipo, kuweni makini katika ukusanyaji wa mapato msikusanywe pesa kutoka kwa Wafanyabiashara wadogo kusanyeni na kwa wakubwa,” amesema Mulongo.

No comments:

Post a Comment