TTCL

EQUITY

Monday, February 16, 2015

MOTO WATEKETEZA MADUKA ENEO LA UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM

Moto  mkubwa uliozuka eneo la Kibangu, Ubungo jijini Dar es Salaam umeteketeza viwanda vya kusaga plastiki, kuchomelea, useremala na kuunguza maduka mawili ya karibu pamoja na vibanda vingine vya biashara eneo hilo. 

Watu walioshuhudia moto huo wamesema moto ulianzia katika kiwanda cha plastiki na baadaye kusambaa maeneo mengine huku wakilaumu kikosi cha zimamoto kuchelewa kufika eneo hilo ambapo baada ya kufika walitaka kuwashambulia kwa mawe lakini Kikosi cha Askari Polisi wakafanikiwa kudhibiti.
 
Eneo hilo linazungukwa na makazi ya watu pamoja na kanisa ambayo hayajaathirika na moto huo.
 
Hapa ni picha kutoka eneo hilo.

No comments:

Post a Comment