TTCL

EQUITY

Saturday, December 6, 2014

Exclusive; Angalia hapa picha mwanamitindo Mtanzania Millen Magese, Kim Kardashian katika muonekano wa vazi moja

Wiki chache zilizopita mwanamitindo wa kimataifa Kim Kardashian alivalia gauni la aina yake linalojulikana kama Atsuko Kudo katika uzinduzi wa perfume yake mpya.Baada yakutokea kwenye red Kapeti akiwa na kivazi hicho kilichovutia wengi,mwanamitindo kutoka Tanzania Millen Magese naye alivalia vazi linalofanana na hilo katika shoo ya mitindo ijulikanayo kama Victoria Secrets fashion show iliyofanyika jijini London, Uingereza.

Gauni hilo lililokua na mwonekano mzuri lilionekana kumvutia mwanadada huyo likiwa limeishia magotini na lilikua na mpasuo nyuma wa kumfanya aweze kutembea vizuri.

Gauni la mwanadada huyo ambaye lilitengenezwa na disgner wake  lilikua maalum kwa ajili ya uzinduzi wa perfume yake mpya ya Fleur Fatale Fragrance katika uzinduzi uliofamyika katika jiji la Melbourne Australia.

Kwa upande wa Millen Magese ambaye alionekana kuvutiwa na vazi hilo naye alivalia vazi linalofanana na ilo sambamba na koti kubwa jeusi.


Achana na akina Masogange na wengineo huyu ndie mrembo mwenye mpododo mkubwa kuliko sema anaishi kijijini

No comments:

Post a Comment