TTCL

EQUITY

Sunday, November 30, 2014

Polisi aliyemuua kijana mweusi ajiuzulu

Raia waandamana Misri

Raia wa Misri waandamana kufuatia kuondolewa mashtaka kwa aliyekuwa rais wa taifa hilo Hosni Mubarak
Vikosi vya usalama nchini Misri vimepambana na karibu waandamanaji 2000 karibu na eneo la Tahrir Square mjini Cairo ambapo mtu mmoja aliuawa.
Maandamano hayo yanafanyika kufuatia uamuzi wa mahakama wa kumuondolea mashtaka aliyekuwa rais wa Misri Honi Mubarak kuhusiana na mauaji ya zaidi ya waandamanaji 200 wakati wa maandamano ya mwaka 2011.
Kweye mahojiano na kituo kimoja cha runinga baada ya hukumu hiyo bwana Mubarak alisema kuwa hajafanya lolote baya.
Mubarak akiwa kizimbani wakati wa uamuzi wa kesi yake.Maelfu ya raia wamefanya maandamano kufuatia hatua ya mahakama kumuondolea mashtaka rais huyo wa zamani.
Awali alihukumiwa kifungo cha maisha gerezani lakini hukumu hyo ikabatilishwa .
Hata hivyo bado yuko kuzuizini baada ya kupatikana na makosa ya ufujaji wa pesa za umma.

Daren Wilson Afisa wa polisi aliyempiga risasi na kumuua kijana mweusi nchini Marekani amejiuzulu.
Wakili wa Darren Wilson ambaye ni afisa wa polisi aliyempiga risasi na kumuua kijana mweusi Michael Brown kwenye eneo la st Louis nchini Marekani mwezi Agosti anasema kuwa polisi huyo amejiuzulu.
Mapema wiki hii bwana Wilson aliondolewa mashtaka hatua iliyozua ghadhabu miongoni mwa waamerika weusi.
Afisa huyo amekuwa likizoni tangu mauji hayo yafanyike, mauaji ambayo yalisababisha majuma kadha ya maandamano.
Michael Brown,kijana mweusi nchini Marekani alipigwa risasi na kuuawa
Gazeti la St Louis limesema kuwa afisa huyo mwenye miaka 28 aliamua kujiuzulu baada ya kitengo chake cha polisi kupokea vitisho kwamba ghasia zitafutia iwapo ataendelea kuhudumu kama mfanyikazi.
Gazeti hilo lilichapisha kile lilichodai kuwa barua yake ya kujiuzulu ambayo ilisoma:''nimearifiwa kwamba iwapo nitaendelea kuwa mfanyikazi wa idara ya Polisi basi hatua hiyo itawachochea maafisa wa polisi na raia wa eneo la Furguson kuishi kwa hofu,hali ambayo siwezi kuikubali hata kidogo.''

No comments:

Post a Comment