Najua
wengi mtakimbilia hapa mana'ke wanawake na ndoa ni kama vile inzi na
kipindu-pindu au kashata na gahawa/kahawa anyway sitokuhakikishai kuwa
nitakachokuambia kitafanya kazi kwani inategemea zaidi na mpenzi wako,
malezi, mazingira,akili yake (yaani how open minded he is) na aina ya maisha yake.
Nakumbuka
siku moja nilikuwa na marafiki zangu fulani (well wadada nimesoma nao
pamoja) mmoja akasema kuwa "James lazima nimfanye anioe" nikajiuliza kwa
sauti kuu huku na cheka (kidhani ni utani) unamfanyaje mwanaume
atangaze ndoa? Ninavyojua mimi ni kuwa mnalizungumzia swala zima kisha
mnasikiliziana kama nyote mna nia moja then siku moja mpenzi (mwanaume
ndio anatangaza ndoa/posa) si ndio....hiyo kisasa.
Ya kizamani ilikuwa binti
unajitahidi kuwa masafi na mwenye tabia njema kisha mwanaume anakuona
kuwa wewe ni "ndoa type" then anakuja kwa wazazi wako kuposa kama sio
wazazi wake wanakupenda kisha wanawashawishi wazazi wako wakubali uolewe
na mwana wao wa kiume alafu from there ndio unaanza kujifunza kama sio
kujilazimisha kumpenda aukumzoea kama mume wako ajae.
Kwa bahati siku hizi tunakuwa kwenye mapenzi na mapendo, kisha tunafanya nusu na robo kama
sio yote yanayofanywa kwenye ndoa lakini jamaa halitangazi ndoa wala
nini na wewe unahisi siku zinakwenda na huna mpango wa kuzaa nje ya
ndoa.
Mwenyewe unajitahidi kumpena na kumuonyesha mapenzi yako, unaongeza
ubunifu kitandani, unampa uhuru/nafasi yake anapohitaji kwenda kulewa
(humfuatilii), mnakwenda kwenye sherehe za ndoa una-comment jinsi
ambavyo siku moja ungependa naninyi mfanye hivyo.....yaani unampa dalili
zote kuwa wewe ni a good wife, lakini Njemba haitangazi ndoa....!
Inaweza ikafikia wakati ukahisi uvumilivu umekushinda na umechoka
kupotezewa muda na hivyo kuchukua uamuzi na kumwambia kama kweli
unanipenda ungefunga ndoa na mimi siku nyingi so ama unanioa ktk wiki
moja au uhusiano umekufa......hapo lazima atatangaza ndoa ili
asikupoteze ikiwa kweli anakupenda au anajua unampenda na hakuna mtu
atakae mpenda kama wewe ila tatizo la hii kitu ni kuwa wewe mwanamke
ndio unaonekanaDesperate kuolewa hivyo unakuwa umelazimisha......ni bonge la noma!
Nikirudi nitakupa mbinuz za kumfanya mshikaji atangaze ndoa na kuifanya
itokee sio mnakuwa wachumba kwa miaka 3 wakati tayari mmeishi pamoja
kama wapenzi kwa miaka 5.....it's boring bana.
Usicheze mbali.
Utachumbiwa lini.........?
Wengi tunaamini kuwa matunda ya mapenzi ni ndoa na sote tunatambua kuwa ndoa ni jambo zuri,
la heshima (wengi wanafeli hapa), busara na chanzo cha familia bora
(japo kuwa mimi siamini sana hapa). Kinachosikitisha ni kuwa huu uamuzi
huwekwa wazi na mwanaume na sio mwanamke hata kama wewe ndio unataka
kuolewa yaani umefika bei n aunajua kabisa Haruna ni
the one lakini Haruna mwenyewe khabari hana (well kama haruna
(muislamu) na haja adopt tamaduni ya watu na yuko karibu au juu ya miaka
25 lazima atatangaza ndoa kwa mujibu wa dini yake) hivyo bora nitumie
jina la Jonathan hahahahaha.
Nimeona hapo chini M2 anasema wanawake tuwe wagumu kutoa K kwani akisha
onja hataki tena, nasikitika kusema kuwa swala la ndoa ni zaidi ya K na
vilevile swala hili linachanganya kiaina. Wakati mwingine mimi huwa
naamini kabisa kuwa ndoa ni mapenzi na uamuzi (labda kwa vile kila
nilietoka nae kama mpenzi alitangaza ndoa), wengine wanadai kuwa ni
bahati na baadhi wanasema ni lazima kama ilivyo ktk kuzaliwa na kufa, si
unakumbuka sherehe 3 hapa duniani kuwa ni kuzaliwa, kuolewa/oa na kufa.
Watu nitakao walenga ni wale ambao wako tayari kwenye uhusiano na
wanapendana lakini wanataka wapenzi wao wawasapuraizi kwa pete ya
uchumba au hata kwenda kutambulishwa kwao kuwa wao ndio wapenzi wa
kudumu.
Mpenzi akifika bei unamjua tu, wala huitaji vithibitisho si ndio jamani?
Lakini mapenzi yake kwako sio tiketi ya yeye kukufanya wewe wa milele
hivyo suibweteke nakusubiri siku akijisikia atangaze ndoa wengine mpaka
uwaonyeshe kuwa "U can live with or without them" ndio wanajisogeza
zaidi, sasa fuata haya yafuatayo:-
1-Ni mwiko kumkutanisha/tambulisha kwaa wazazi wako au kumpa namba ya
simu ya nyumbani kama sio ya baba na mama (ya wazungu waachieni wenyewe)
haruhusiwi kuwazoea bila kuji-commit. Kumbuka kuwa mwanaume anatakiwa
kulifanyia kazi hili na kuhakikisha kuwa anakutana na wazazi wako
nakujitambulisha ikiwa tu pete iko kidoleni na mnakwenda huko
kutambulisha uchumba rasmi nakufuata taratibu nyingine za mahari, barua
n.k. sio mmekutana leo kesho yuko sebuleni angalia Tv au kucheza na
wadogo zako kama sio kuwapeleka kwenye manunuzi pale soko mjinga au
kwenye maonyesho ya saba-saba.
Kama kwa bahati mbaya tayari amekwisha kutana na wazazi wako kabla ya
makala yangu hii basi hakikisha hapati tena nafasi hiyo,mpaka kuwepo na
pete au hata yeye kuandika barua nakulipa mahali nusu na robo (mana'ke
sio wote wanaamini ktk pete).
Ikitokea shughuli kubwa kwenye Ukoo wenu kama vile sherehe za ndoa au
Msiba hakikisha unakwenda mwenyewe bila yeye, ofcoz unamwambia nini
nimetokea (msiba)au kinakwenda kutokea(ndoa) na akiomba kushiriki au
kwenda na wewe mwambie ungependa awepo lakini hudhani kuwa ni wazo zuri
kwani utakuwa busy sana (hutokuwa na muda wa kuwa pamoja kama wapenzi)
na sio hivyo tu bali unajaribu kum-save na too much hassle.....hapa
atakuona wewe ni wa maana sana nakuna uwezekano mkubwa siki za karibuni
akataka uwe wake wa daima milele(Daima).....Usisahau kuwa hayuko pale
kupendwa na ndugu zako na wala haitaji kupenda na kuzoea nyumbani kwenu.
2-Kamwe aah ni marufuku kuhamia kwake au yeye kuhamia kwako ikiwa kila
mmoja wenu anajitegemea (anaishi kwake), wengi hukimbilia ku-move in
wakihofia wapenzi wao kuchukua watu wengine na kulala nao.....skia wewe,
achakuwa tegemezi kihivyo (emotional) utakimbiwa, kila mtu anahitaji
nafasi yake time to time, swala la kulala na mtu mwingine kama lipo basi
anaweza na mtu huyo hotelini, nyumba za kulala wageni au hata ofisini
wakati kila mtu katoka....swalamuhimu ni mapenzi ya dhati na uaminifu.
Ikiwa ulihamia kwake ili ukamuonyeshe umuhimu wako kama "mke" yaani
kupika, kusafisha, kupiga basi, kumpangia nguzo shati na tai nzuri kwa
ajili ya kazini n.k. na bado Njemba haina dalili yakutangaza ndoa basi
ni wakati wa kuhamia kwako peke yako kama sio kurudi kwa dada/wazazi, na
kumbuka unapo hama bakiza kachupi kako kadogo ambako anakapenda kukaona
maungoni mwako.
Ukihamia kwa mpenzi wako kabla ya kuchumbiwa, itamafanya ajisahau
navilevile atakujua kwa sana yaani mambo mengine ulitakiwa uyafanye
baada ya miaka 5 yandoa wewe unayafanya kabla hata ya uchumba na nina
kuhakikishia ndoa haitoangazwa unless baba na mama'ke wamwambie "hey
bwan' mdogo unataka tufe kabla hatujamuona mkwe na mjukuu "ndio atatuma
posa? Yaleyale......!
Kuhamia kwake kunaruhusiwa ikiwa tu ametangaza ndoa na maandalizi ya
ndoa yameanza (tunaita trial), alafu mwezi mmoja kabla ya ndoa unarudi
kwenu....sio kwako....kwenu kwa wazazi au ndugu.
3-Ni mwiko kujifananisha ninyi na pea inayo au iliyofunga ndoa hivi
karibuni, yaani wewe unatakiwakua "nunda" when it comes kwenye maswala
ya ndoa au uchumba wa watu wengine, hasa kama yeye anaonyesha kutokuwa
na habari (kawaida wanaume huwa hawana habari wala wivu) basi na wewe
kuwa kama yeye.
Siku umeenda kumtembelea Mpenzi amabe kafika bei ila swala la ndoa
halipo eti mpaka ajenge nyumba......lini? (kumbuka hakuna kuishi pamoja
mpaka achumbie)ukiwa unaongea na rafiki yako amabe kafunga doa hakikisha
unasema sentensi za kuponda ndoa kwa sauti ili mpenzi asikie tena kwa
kunogesha muulize "hivi inakuwaje unaweza kuishi na mtu yuleyule kila
siku iendayo kwa Mungu?" Mimi sidhani kama nitaweza, nahisi itakuwa
boring"......hehehe kwa yote unayomfanyia nakumridhisha kitandani, kwa
jinsi unavyompenda na kumjali alafu anasikia hivyo.....yaani akili
itamjia Njemba nyingine zinaweza niwahi hapa......ataenda itafuta pete
ktk siku zijazo, wewe subiri tu.
Hakikisha unayasema yote hayo kuwa unajua kabisa anakupenda kwa dhati na maisha bile wewe ni bora kifo.....mana'ke ukisema haya kwa player ujue kashinda na atakung'ang'ania na pete usiione alafu anaenda kuoa mtu mwingineee.
No comments:
Post a Comment