TTCL

EQUITY

Saturday, February 16, 2013

ZIFAHAMU DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI NA TIBA YAKE

Unapokuwa na tatizo la sukari, unatakiwa kujua jinsi ya kuishi kila siku ili kuepukana na tatizo hilo. Kiasi ambacho hata mpenzi wako ataacha kuogopa kuhusu hali yako. Kiasi kwamba afya yako itakuwa katika hali nzuri. Kiasi hicho cha sukari katika damu yako kiwe kinapungua kila siku na kupelekea afya yako kurudi katika hali ya kawaida.
Vitu ambavyo vinaweza kuongeza au kukuletea shida ya ongezeko la sukari kwenye damu yako ni pamoja na dalili za kuwa na sukari ni
·         Kuongezeka uzito
·         Tamaa ya kula vitu vya sukari au sukari yenyewe.
·         Kuishiwa nguvu
·         Kukojoa kila mara
·         Kuwa mchovu
·         Kuwa na kiu
·         NK
Hizi ni dalili ambazo zinaashiria kiwango cha sukari katika damu yako kinaweza kuwa juu.
Kuongeza kwa kiwango cha sukari katika damu yako mara kwa mara kunaweza kukuletea matatizo mengi ya kiafya, yakiwepo
·         Magonjwa ya moyo.
·         Matatizo ya macho.
·         Matatizo katika figo
·         Kukosa hamu ta tendo la ndoa au kushindwa kabisa.
Na mzunguko mzima wa mwili wako kuwa na matatizo mengi.  Haya ni baadhi ya mambo yanayotokea wakati kiwango cha sukari kwenye damu kiko juu.
CHUNGA UNACHOKULA
Kuchunga au kujua unachotakiwa kula ni sehemu ya matibabu ya tatizo hili la ongezeko la sukari katika damu. 
Hii ndio maana CORNWELL TANZANIA tumekutengenezea  DIEBETIC PROGRAM  ambayo itakusaidia kupunguza tatizo hili au kuondoa kabisa. Kukupa nguvu ya kuweza kuishi maisha ya kawaida. Pia kuwa na elimu ya afya. 
Ndani ya siku 30 utaweza kuona tofauti kubwa kiafya na kiakili pia. Mwili wako utakuwa na uwezo wa kuvunja huo mzunguko mmbaya wa sukari kwenye damu.
Siyo tu hivyo, ila pia utafurahia faida ya kuwa na hamu ya kula. Kuwa na kumbu kumbu pia na hamu ya Tendo la ndoa na vitu vingine vingi ambavyo hushindwa kufanywa wakati sukari inapokuwa juu.
Usingoje mpaka kiwango cha sukari kwenye damu yako kiwe juu. Jifunze kucheck afya yako kila mara. CHUNGA UNACHOKULA. JUA UNACHOTAKIWA KULA NA NI WAKATI GANI. 

No comments:

Post a Comment