Jeneza
lenye Mwili wa Marehemu Dotto Mzava likishushwa Kwenye gari maalum mara
baada ya kuwasili katika kanisa la Wasabato Manzese uzuri kwaajili ya
sala ya kuombea kabla ya Mwili kusafirishwa kuelekea Wilaya ya Same
Mkoani Kilimanjaro.
Mchungaji
wa kanisa la Adventist wasabato akiendelea na ibada wakati wa ibada ya
kumuombea marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Jamii Media Maxence Mello akitoa historia fupi
ya Marehemu Dotto Mzava ambae pia alikua mmoja wa watumishi katika
kampuni hiyo.
Baba
Mkubwa wa marehemu Dotto Mzava akitoa maneno ya shukrani katika kanisa
la Kisabato la Manzese Uzuri mara baada ya zoezi la misa kumalizika.
Heshima za Mwisho zikiendelea kutolewa
Majonzi na simanzi kwa ndugu wa marehemu
Mmiliki wa Fullshangwe Blog,John Bukuku akitoa heshima za mwisho
Heshima
za mwisho zikiendelea kutolewa kwa mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla
haujasafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwaajili ya mazishi
Mbunge
wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika akitoa heshima zake za mwisho kwa
mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla ya Kusafirishwa kuelekea Same
Kilimanjaro kwa mazishi yanayotarjiwa kufanyika kesho
Mkurugenzi
mtendaji wa Jamii Media akitoa heshima za mwisho kabla ya mwili wa
marehemu kusafirishwa Same Mkoani Kilimanjaro mapema leo
No comments:
Post a Comment