TTCL

EQUITY

Saturday, May 3, 2014

CCBRT- MOSHI YAWAPATIA VIJANA WENYE ULEMAVU MAFUNZO YA UJASIRIA MALI, KILIMO, ELIMU YA UZAZI NA KUJAMIIANA.


Mratibu wa mafunzo ya vijana Bw. Shadrack Domingo (wanne kutoka kusho kwa walio kaa) akielezea kwa lugha ya kiswahili kile kilichokuwa kikizungumzwa na wawezeshaji ambapo walikuwa wakizungumza kiingereza
Vijana wenye ulemavu wa kichwa kikubwa na mgongo wazi wamepatiwa mafunzo ya wiki moja nakukamilisha sehemu ya kwanza ya mafunzo wanayohudhuria mara mbili kwa mwaka ambapo wamejifunza Ujasiriamali, Kilimo Jikoni, Elimu yauzazi, Kujamiina pamoja na msongo wa mawazo, mafunzo hayo yalifanyika jumatatu tarehe 28/04/2014 nakumalizika tarehe 2/05/2014 CCBRT - Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Mratibu na kiongozi wa shughuli za vijana wenye ulemavu wakichwa kikubwa na mgongo wazi Bw. Shadracky Domingo amekuwa akifuatilia kwa makini mafunzo hayo na kujifunza nao lengo ikiwa nikutakakufahamu namna walemavu wanavyoweza kuzitumia fursa watakazo ambiwa na wakufunzi, amesema kwa mujibu wa mafunzo anahakika ikiwa vijana hao watajiamini na kuwa na uthubutu watafanikiwa.

Mmoja wa vijana walioshiriki mafunzo Bw. Emmanuel Lymo ametoa ushauri wake nakusema “walemavu wanatakiwa kujikubali, kuwa wenyekuamua na kutenda” aliongeza kusema kuwa ulemavu haidhuru kuwa na mafanikio, alimalizia kwakusema wapo watu wengi wenye ulemavu ni maarufu, wakiwemo viongozi wa nchi, na wengine wataalamu wa teknolojia wanamaendeleo na mafanikio makubwa, kwao watu hao ingefaa kuwa mfano wa kuigwa.
Baadhi ya wawezeshaji wakiwa wanasikiliza kwa makini wenzao wakati wa mafunzo (hawapo pichani).
Mkufunzi wa ujasiriamali Bw. Issac Ara wakati yeye akihitimisha mafunzo yake aliwataka vijana kuamua kuthubutu, kujiamini na kuwa wenye malengo timilifu. Akielezea sifa za mjasiriamali aliwashirikisha kila mmoja katika kumtaka aeleze ni namnagani anaelewa tofauti za mjasiriamali na ujasiriamali, pia aliwaeleza fursa walizonazo ni nyingi hivyo nikujiamini na kuchukua hatua.

Vilevile alifundisha kuwa kwakila wazo yafaa kuliweka kwenye uso wa karatasi, akimaanisha  kuliandika lile mtu unaloliwaza kufanya, au umiliki kama mradi, biashara ama taasisi. Pia alieleza namna yakuandaa wazo, kuliweka katika uso wa karatasi, kuandika na kuweza kuwa biashara kamili yenyekuingiza kipato. Bw. Ara alimalizia kwakumkaribisha mwenyeji na mratibu wa mafunzo ya vijana hao Bw. Domingo ilikuweza kuhitimisha shughuli hiyo.

Bw. Domingo aliwataka vijana kutoa maoni yao kwakilewalichojifunza, pia aliwapa fursa ya kuchagua aina mpya ya mafunzo ambayo wangehitaji kuyapata katika awamu ya pili watakaporudi tena mwezi wa (12) Disemba mwaka huu. Aidha kila mmoja aligawiwa mbegu za mbogamboga ili kwenda kuotesha kwao, ikiwa kama sehemu ya mafunzo ya vitendo ya kilimo darasani.

Wawezesha wa mafunzo ya wiki ya vija wenye ulemavu wakiwa katika picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment