Fred Nyman - mwanzilishi wa RHM
Historia ya Redio Habari Maalum
RHM (Redio Habari Maalum) kwa sasa Habari
Maalum media. Ni studio inayoshughulika na uandaaji wa vipindi vya
Redio ambavyo vinarekodiwa na kurushwa katika Stesheni
mbalimbali. Habari Maalum Media iko kilometa kumi na tano (15km)
Kaskazini mwa mji wa Arusha barabara iendayo Nairobi kupitia Namanga.
Mwanzilishi wa kazi hii ni Mchungaji Fred Nyman kutoka Finland. Lengo
kuu la kuanzishwa kwa Redio Habari Maalum ni kuwafikia watu kwa injili,
wapatao milioni 70 wanaozungumza kiswahili katika eneo la Afrika
mashariki na kati. Maandalizi ya kipindi cha kwanza yalianza kwenye
miaka ya sitini. Tarehe 05/09/1976, kipindi cha kwanza cha dakika kumi
na tano kilirushwa na FEBA Radio huko Seychelles kupitia masafa mafupi
au short wave (SW) na mtangazaji wa kwanza aliyetangaza kipindi hicho
alikuwa Mchungaji Fred Nyman wa Finland ambaye kwa sasa ni mchungaji
nchini Finland.
Habari Maalum Media
Habari Maalum Media (HMM) ni mojawapo
kati ya idara zilizopo chini ya kanisa la Free Pentekoste Church of
Tanzania (FPCT). Habari Maalum Media tunashughulika na Uandaaji wa
vipindi vya Redio na Televisheni ambavyo vinarekodiwa katika studio zetu
na kurushwa katika Stesheni mbalimbali za Redio na Television ndani na
nje ya Nchi ya Tanzania.Habari Maalum Media tunaendesha kozi mbalimbali
kama kozi za Uandaaji na Utangazaji wa vipindi vya Redio naTelevisheni (MPT)
pamoja na kozi za Mazingira. Tunarekodi nyimbo katika Audio na Video
kwa kutumia vifaa vya kisasa na kwa ubora wa hali ya juu. Kutokana na
studio ya kisasa tuliyonayo na vifaa vya kisasa vya "digital Audio and
Video Recording " tunaweza turekodi nyimbo katika Audio na Video kwa
ubora wa hali ya juu na kuweza kukupatia wewe nyimbo bora katika CD,
Kaseti, kanda za Video (VHS tapes) na DVD.
No comments:
Post a Comment