TTCL

EQUITY

Tuesday, March 1, 2016

CCM iheshimu mfumo wa vyama vingi - Dkt Bana

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumzia suala la upatikanaji wa Meya wa jiji la Dar es salaam ambapo limegubikwa na mambo ya siasa zizizofaa kwa maendeleo ya wananchi na wapenda demokrasia nchini.
''Kauli za mvutano na malumbano ya UKAWA na chama cha mapinduzi havitasaidia wananchi kwanza wanajidhalilisha kinachotakiwa ni upinzani kutumia busara lakini chama tawala pia watambue kwamba walipokubali mfumo wa vyama vingi lazima wakubali mabadiliko na kuheshimu mfumo wa vyama vingi”
Hakuna sababu ya msingi ya kuwepo malumbano hadi watu wengine wapigwe na wengine kuwekwa rumande kwanza kazi kubwa ya umeya ni kuongoza vikao ingelikuwa tunatafuta mkurugenzi hapo sawa lakini hili wanakosea kwa kweli''-Amesema Dkt. Bana
Meya wa jiji la Dar es salaam ameshindwa kuchaguliwa mara kadhaa pamoja na kuwepo kwa uhalali wa kufanyika uchaguzi huo jambo ambalo limesababisha malumbano makali na kushikiliwa kwa wabunge wawili wa Chadema Saed Kubenea na Halima Mdee.

No comments:

Post a Comment