TTCL

EQUITY

Saturday, January 30, 2016

TAMWA KUJADILI YALIYOJIRI KWENYE KONGAMANO LA AFRIKA.

Mkurugenzi mtendaji wa Chama cha wanahabari wanawake Tanzania-TAMWA- Valerie Msoka akizungumza na Mwandishi wetu alipomtembelea ofisini kwake.
CHAMA cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) kwa kushirikiana na Ubalozi wa Canada nchini, leo utafanya mkutano wa siku moja kujadili yaliyojiri katika kongamano la nchi za Afrika lenye lengo la mpango mkakati uliojadiliwa kwa ajili ya kutokomeza mimba za utotoni lililofanyika Desemba, 2015 Lusaka nchini Zambia.
Mkutano huo utakaofanyika katika ofisi za Tamwa Sinza Mori, Dar es Salaam, utahusisha pia wadau mbalimbali wanaopigania haki za watoto, kujadili ufanisi na utekelezaji wa sheria zilizopo ili kuweka mpango mkakati wa kulaani ndoa za umri mdogo Tanzania na jinsi ya kusonga mbele.
Mkutano huo utajenga imani ya pamoja kutokana na maazimio ya kongamano la Umoja wa Nchi za Afrika kwa kuwa Tanzania inatambua kuwa kutokomeza ndoa za utotoni kunahitaji dhamira ya kisiasa, yenye maono na uwezo wa kuongoza, ushiriki wa wadau mbalimbali, watoto, pamoja na uwezeshaji katika kupinga mila kandamizi kuanzia ngazi za chini ili kubadilisha taratibu ambazo husababisha kuongezeka kwa ndoa za umri mdogo.

No comments:

Post a Comment