TTCL

EQUITY

Wednesday, January 13, 2016

Serikali Yampa Zawadi Nono Samatta

Samatta Waziri Mkuu (4) 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi (kulia), Mbwana Samatta (kushoto) sambamba na viongozi mbalimbali wa serikali na wadau soka wakiingia kwenye ukumbi wa Hyatt jijini Dar jana usiku kwenye hafla ya kumpongeza Samatta.

Samatta Waziri Mkuu (5) 
Kutoka kulia ni Waziri Lukuvi, Mbwana Samatta na Waziri wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye.

Samatta Waziri Mkuu (6) 
Samatta katika picha ya pamoja na Wazriri Nape, Waziri Lukuvi na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi (kulia).
 
IKIWA ni kuthamini tuzo aliyotwaa nahodha wa timu taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ya Mchezaji Bora wa Soka Afrika kwa wachezaji wa ndani, Serikali kupitia wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, jana imemzawadia nyota huyo kiwanja cha kujenga makazi kilichopo eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kujali na kuthamini heshima ambayo Samatta ameiletea Tanzania ya kuwa mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani (ligi za Afrika).
Samatta amepewa kiwanja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi kwenye sherehe maalum ya kumpongeza Mbwana Samatta kwa kutwaa tuzo hiyo iliyoipa heshima kubwa Tanzania, jana usiku  Hyatt jijini Dar es Salaam.
Mbwana Samatta aliishukuru serikali kwa kutambua mchango wake katika soka la ndani, sapoti ya serikali katika masuala ya soka na michezo kwa ujumla huku akiiomba serikali kuweka mikakati endelevu ya kuendeleza soka nakuibua vipaji zaidi ili wapatikane akina Samatta wengi zaidi.
Kwa upande mwingine, Samatta aliwashukuru Watanzania na wadau wote wa michezo wanaomuunga mkono.  Samatta amesema amekuwa akifarijika tokea arejee nyumbani na tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika anayecheza Afrika kutokana na Watanzania kuendelea kumfariji.
“Naendelea kusema tena ninashukuru kwa sapoti yenu, najua nimesema hivi mara kadhaa. Lakini si vibaya kushukuru tena” alisema.
Samatta amezidi kuwa gumzo na lulu baada ya kufanikiwa kutwaa tuzo hiyo ya mwanasoka bora Afrika na kuweka rekodi mpya Tanzania.
Samatta Waziri Mkuu (7)  

Lukuvi (kushoto) na Samatta wakiteta jambo.

 Samatta Waziri Mkuu (8) Samatta Waziri Mkuu (9)  
…Hafla hiyo ikiendelea

 Samatta Waziri Mkuu (1)Samatta Waziri Mkuu (10) Samatta Waziri Mkuu (11) Samatta Waziri Mkuu (13) Samatta Waziri Mkuu (14)  
Rais wa TFF, Jamal Malinzi akizungumza

Samatta Waziri Mkuu (15)
Samatta akitoa neno la shukrani kwa Serikali na Watanzania wote kwa kumsapoti.
Samatta Waziri Mkuu (18)
Waziri wa Vijana, Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mh. Nape Nnauye akimpongeza Samatta kwa mara nyingine.
Samatta Waziri Mkuu (19)
 Mgeni rasmi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akimpongeza Samatta.
Samatta Waziri Mkuu (21) Mgeni rasmi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kwa niaba ya Waziri Mkuu, kassim Majaliwa akikabdhi zawadi kwa Samatta.

 Samatta Waziri Mkuu (22) Samatta Waziri Mkuu (23)  
Samatta akikabidhi jezi yake kwa Waziri Lukuvi
 Samatta Waziri Mkuu (24)Samatta akikabidhi jezi yake kwa Waziri Nape
 Samatta Waziri Mkuu (25) Samatta Waziri Mkuu (26) Samatta Waziri Mkuu (27) Picha za pamoja na viongozi wa serikali na wadau wa soka
 Samatta Waziri Mkuu (3)
Mhariri Kiongozi wa Gazeti la Championi, Saleh Ally (kulia) akibadilishana mawazo na mmoja wa wadau waliofika pale.
 Samatta Waziri Mkuu (16)
Samatta Waziri Mkuu (28)
Samatta Waziri Mkuu (31) Thomas Ulimwengu akisalimiana na baba wa Mbwana Samatta, mzee Samatta
 Samatta Waziri Mkuu (32)  Samatta Waziri Mkuu (34) …Picha ya pamoja na wadau.
 Samatta Waziri Mkuu (35) 
Kutoka kushoto ni Mshindi wa Big Brother Africa (BBA) 2014/2015, Idris Sultan, Mbwana 
Samatta Waziri Mkuu (37)
MBWANA SAMATTA NA THOMAS ULIMWENGU

No comments:

Post a Comment