Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi (kulia), Mbwana Samatta (kushoto) sambamba na viongozi mbalimbali wa serikali na wadau soka wakiingia kwenye ukumbi wa Hyatt jijini Dar jana usiku kwenye hafla ya kumpongeza Samatta.
Kutoka kulia ni Waziri Lukuvi, Mbwana Samatta na Waziri wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye.
Samatta katika picha ya pamoja na Wazriri Nape, Waziri Lukuvi na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi (kulia).
IKIWA ni kuthamini tuzo aliyotwaa
nahodha wa timu taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ya Mchezaji Bora wa
Soka Afrika kwa wachezaji wa ndani, Serikali kupitia wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, jana imemzawadia nyota huyo kiwanja cha
kujenga makazi kilichopo eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam ikiwa ni
sehemu ya kujali na kuthamini heshima ambayo Samatta ameiletea Tanzania
ya kuwa mwanasoka bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani (ligi
za Afrika).
Samatta amepewa kiwanja na Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi kwenye sherehe
maalum ya kumpongeza Mbwana Samatta kwa kutwaa tuzo hiyo iliyoipa
heshima kubwa Tanzania, jana usiku Hyatt jijini Dar es Salaam.
Mbwana Samatta aliishukuru serikali kwa
kutambua mchango wake katika soka la ndani, sapoti ya serikali katika
masuala ya soka na michezo kwa ujumla huku akiiomba serikali kuweka
mikakati endelevu ya kuendeleza soka nakuibua vipaji zaidi ili
wapatikane akina Samatta wengi zaidi.
Kwa upande mwingine, Samatta
aliwashukuru Watanzania na wadau wote wa michezo wanaomuunga
mkono. Samatta amesema amekuwa akifarijika tokea arejee nyumbani na
tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika anayecheza Afrika kutokana na Watanzania
kuendelea kumfariji.
“Naendelea kusema tena ninashukuru kwa sapoti yenu, najua nimesema hivi mara kadhaa. Lakini si vibaya kushukuru tena” alisema.
Samatta amezidi kuwa gumzo na lulu baada ya kufanikiwa kutwaa tuzo hiyo ya mwanasoka bora Afrika na kuweka rekodi mpya Tanzania.
Lukuvi (kushoto) na Samatta wakiteta jambo.
…Hafla hiyo ikiendelea
Rais wa TFF, Jamal Malinzi akizungumza
Samatta akitoa neno la shukrani kwa Serikali na Watanzania wote kwa kumsapoti. |
Waziri wa Vijana, Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mh. Nape Nnauye akimpongeza Samatta kwa mara nyingine. |
Mgeni rasmi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akimpongeza Samatta. |
Mgeni
rasmi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi
kwa niaba ya Waziri Mkuu, kassim Majaliwa akikabdhi zawadi kwa Samatta.
Samatta akikabidhi jezi yake kwa Waziri Lukuvi
Samatta akikabidhi jezi yake kwa Waziri Nape
Picha za pamoja na viongozi wa serikali na wadau wa soka
Mhariri Kiongozi wa Gazeti la Championi, Saleh Ally (kulia) akibadilishana mawazo na mmoja wa wadau waliofika pale.
Thomas Ulimwengu akisalimiana na baba wa Mbwana Samatta, mzee Samatta
…Picha ya pamoja na wadau.
Thomas Ulimwengu akisalimiana na baba wa Mbwana Samatta, mzee Samatta
…Picha ya pamoja na wadau.
Kutoka kushoto ni Mshindi wa Big Brother Africa (BBA) 2014/2015, Idris Sultan, Mbwana
MBWANA SAMATTA NA THOMAS ULIMWENGU |
No comments:
Post a Comment