TTCL

EQUITY

Wednesday, September 30, 2015

HOJA YANGU: KWA UWAJIBIKAJI NA UADILIFU HUU WA MH. KINABO KUNAYO HAJA YA THEMI KUMPA RIDHAA YA KUONGOZA UNGWE YA PILI KWA MWAKA 2015 – 2020.



Mh. Melance E. Kinabo (anayetetea kiti chake cha udiwani)

 Themi ni miongoni mwa kata zeyenye rasilimali nyingi ikiwemo viwanda na uwanja wa maonesho ya siku ya wakulima (nane nane), Wakati Jiji la Arusha likitajwa kushikilia nafasi ya kwanza kwa  usafi kati ya Majiji yote Tanzania kwa mara ya kwanza, Themi nayo imekuwa miongoni mwa kata zilizo tajwa kuongoza kwa usafi 2013 - 2014 chini yauongozi wa Mh. Diwani Melance Kinabo, ikishikilia nafasi ya pili ndani ya halmashauri.

Robo tatu ya wakazi wa Themi sawa na 60% ni wafanyakazi wa viwandani na wengine waliobaki ni wafanyakazi katika maeneo mbalimbali. mwaka 2008 wafanyakazi wa kiwanda kilichokuwa kikizalisha matairi bora afrika mashariki walipewa taarifa ya kusimama kazi kwa madai kuwa kiwanda amepewa mwekezaji, jambo ambalo liliathiri wakazi wengi wa themi waliokuwa wakitegemea ujira huo kuendesha maisha yao.

Themi imebarikiwa kwa kuwa na viwanda vingi ikiwemo ABB, Kilitex, Sunflag, A to Z, Breweries, Genera tire n.k ambapo hivi sasa vingi vimeuwawa na serikali tawala baada ya kukabidhi wawekezaji na sasa kugeuka kuwa maskani ya vibaka na wacheza kamari, na kimojawapo kugeuzwa eneo la kanisa.

Ujio wa Mh. Melance Kinabo umekuwa ni faraja kubwa kwa Themi, amabapo aliongoza kwa kipindi cha miezi michache baada ya kuenguliwa kwa madiwani wanne wa chadema waliobainika kuwa walikuwa wakitumiwa na CCM baada ya kupokea rushwa kwa lengo la kumpitisha Meya wa Jiji la Arusha kutoka CCM.

Katikati ni Mh. Diwani wa kata ya Themi wakati akikabidhi Solar (umeme wa jua) katika kituo cha Afya Themi
 Mh. Kinabo katika kipindi kifupi cha uongozi wake amefanikiwa katika maeneo mbalimbali nayo ni;

Elimu
Mh. Kinabo amefanikiwa kuanzisha mpango maalum wa kusomesha watoto 2000 wanaotoka katikafamilia duni, kutoka shule za sekondari 10, na shule za msingi 10.
Na katika elimu yapo maeneo mawili ambayo ameyashughulikia, ambapo ni shule za msingi na sekondari.

Shule za msingi
Shule ya msingi Engira mh. Kinabo amefanikiwa kutekeleza robotatu ya ahadi zake zote ikiwemo,
Uchimbaji wa kisima cha maji na ufungaji wa pampu ya kupandisha maji, ambapo imepunguza adha kubwa ya upatikanaji wa maji kwaajili ya mazingira ya shule na mahitaji kwa wanafunzi.
Ujenzi na ukarabati wa madarasa mawili, ambapo yamejengwa kisasa zaidi na kugawanywa mawili kuwa ukumbi wa mikutano na lingine kuwa darasa maalumu la kompyuta.
Kurudisha umeme wa shule na kufanya baadhi ya shughuli zinazohitaji umeme kufanikiwa, kutokana na sehemu kubwa ya elimu na maisha ya sasa kutawaliwa na teknolojia.
Ukarabati wa choo cha matundu manne cha maji jambo ambalo limeifanya shule ya Engira kuonekana maridadi na haa kuwa vutia wanafunzi.
Aidha ufaulu wa wanafunzi wa Engira ulipanda kwa 100% 2013-2014, ambapo Mh. Diwani amekuwa akionesha ushirikiano katika kila hatua hususa kufadhili ziara za mafunzo mf. Ziara ya kutembelea hifadhi za wanyamapori ikiwemo Ngorongoro.

Shule ya msingi Themi pia Mh. Diwani amefanikiwa kutekeleza machache ikiwemo,
Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, na ununuzi wa mashine maalumu kwa ajili ya watu wasioona (Vipofu).
Ukarabati wa madarasa, na utengenezaji mashelfu kwaajili ya kuhifadhi vifaa vya masomo.
Ufaulu wa wanafunzi umeongezeka na kufikia 100% 2013-2014.

Shule za Sekondari
Shule ya sekondari Themi Mh. Diwani ametekeleza ahadi zake kwa zaidi ya asilimia 80%.
Ujenzi wa maabara tatu za kisasa
Upatikanaji wa eneo jipya la shule
Ukarabati na ununuzi wa vifaa vya shule ( ikiwemo madawati na viti)
Ujenzi wa geti na uzio wa shule
Ukamilishwaji wa ujenzi wa marasa manne ya ghorofa.
Kwa kiwango hicho mh. Diwani amechochea kusukuma maendeleo makubwa ya shule ya sekondari Themi, pia amekuwa akiwaombea wanafunzi misaada ya kiamasomo kupitia wadau mbalimbali, Taasisi za umma na Binafsi, ambapo ongezeko la ufaulu limekuwa kwa zaidi ya 65%

Shule ya Sekondari Arusha Day umefanyika ukarabati wa ofisi ya waalimu na maabara mbili, pamoja na ujenzi wa maabara nyingine ya kisasa, ujenzi wa uzio na geti la shule, pamoja na ujenzi wa kivuko cha waenda kwa miguu kwa usalama wa wanafunzi na raia wengine.

Afya
Uwekwaji wa sola (umeme wa juwa) kituo cha afya imegharim, Pia kwa juhudi za Mh. Diwani umefanyika ukarabati wa vyoo na kuvifanya kuwa na miondombinu rafiki kwa wagonjwa. Uhamasishaji kwa kila familia kujiunga na afya ya jamii tiba kwa kadi (TIKA) inayogharimu Tsh. 12,000/= kwa mwaka. Aidha kwakutambua umuhim wa jamii na afya zao, Mh. Diwani amekuwa mstari wa mbele kutete huduma za afya kufanyika hadi siku ya jumamosi mpangoa ambao kwasasa umeridhiwa, Mh. Amehakikisha huduma ya mama na motto inakuwa salama na hivyo amekipatia kituo cha Afya Themi kitanda maalum na cha kisasa kwaajili ya kujifungulia akinamama wajawazito.

VIKUNDI
Vikundi vya akinamama kwa kuanzisha mradi wa akinamama Themi living garden, mradi huu unawasaidia akinamam wanaoishi kwenye mazingira hatarishi, aidha umefanyika mchakato wa upatikanaji wa (12. M) kwaajili ya kuwakopesha vijana, na akinamama. Katika awamu ya Mh. Kinabo kumekuwa na ongezeko kubwa la uanzishwaji wa vikundi vya wajasiriamali katika Nyanja mbalimbali mfano vikundi vya sanaa, kuweka na kukopa n.k (kutoka vikundi 7, hadi kufikia 21).

MIUNDOMBINU
Umefanyika ukarabati wa ofisi ya Afisa mtendaji kata ya Themi na kurejeshwa umeme uliokuwa umekatwa kutokana na deni lililokuwepo hapo awali. Pia umefanyika ukarabati wa barabara za mitaa ya naenane, kambini, barabara ya Biya, kambarage, na ukarabati wa Barbara ya lami kutoka reline hadi uhasibu, kwa ushirikiano na kata ya Olorieni Mh. Amefanikiwa kujenga kivuko cha mtaa wa kambarage. Kufunguliwa na kutumika Barbara ya mount meru kupitia mahakama kuu, iliyokuwa imefunwa kwa muda mrefu.

HALMASHAURI
Ukuwaji wa mapato ya halmashauri kutoka 500 Million hadi 1.3 Billion.
Kufanya ushawishi wa serikali kununua mitambo maalumu kwaajili ya ujenzi wa miundombinu grader 1, compactor machine 1, na malori 3, kupatikana kwa hati safi baada ya miaka 5 ya hati zenye mashaka. ununuzi wa gari la wagonjwa (Ambulance), kushawishi na kutetea Arusha kuingizwa ktk (Master plan) mpango maalumu wa kuendeleza jiji la Arusha.
Haya ni miongoni mwa mafanikio ya Mh. Melance Kinabo katika kipindi chake cha uongozi, hivyo kwa kasi hii, uwezo na uthubutu aliouonesha ni dhahiri anakilasababu ya kupewa dhamana ya kurejea ili kuendelea kukamilisha mengine aliyoahidi na kukosa muda wa kutekeleza yote.
Themi inahitaji kurejesha heshima yake, kata hii inautajiri mwingi na iwapo serikali itakuwa makini katika kusimamia na kuweka mikakati yake vyema Themi inauwezo wakutengeneza zaidi ya 65% ya ajira kwa vijana wengi waliopo nchini wasio na ajira, pia inaweza kuwa kata pekee yenye kuchangia pato kubwa la Halmashauri kutokana na wingi wa viwanda vyake vilivyo uawa na wawekezaji.

Kwa kuzingatia sifa za uongozi bora Mh. Melance Kinabo ndiye  kiongozi mwana harakati na mtetezi wa Themi, kwakua anayoniya, uthubutu, sauti ya umma, msemaji na mtendaji mwaminifu.

No comments:

Post a Comment