TTCL

EQUITY

Monday, March 2, 2015

Utafiti:Wanawake huwa na mpango m'badala

Wapenzi wawili

Nusu ya wanawake huwa na mpango mbadala ama wa kando ambao wanaweza kukimbilia iwapo uhusiano wao utaharibika.
Utafiti uliofanywa miongoni mwa wanawake 1000 uligundua kuwa asilimia kubwa imeweza kuwaweka wanaume mbadala pindi tu uhusiano walionao unapoharibika.
Cha kushangaza ni kwamba wanawake waliomo katika ndoa huwa na mpango mbadala ikilinganishwa na wale walio katika uhusiano wa kawaida.
Pia imebainika kuwa mpango huo wa kando huenda akawa rafiki wa zamani ambaye amekuwa akimpenda mwanamke huyo.
Wengine huwa wapenzi wa zamani ama hata mume waliyeachana naye,rafiki ama mtu ambaye walikutana katika eneo la mazoezi.
Utafiti huo ulifanywa na kampuni ya utafiti wa mtandaoni wa Onepoll
Je, unakubaliana na utafiti huu? Kwa maoni yako ingia katika mtandao wetu wa facebook sweetness of affenction

No comments:

Post a Comment