TTCL

EQUITY

Thursday, January 8, 2015

Magari yenye picha za rais yakamatwa

Gari la kubeba abiria lililochorwa picha ya rais Uhuru Kenyatta
Licha ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuruhusu magari yanayobeba abiria nchini Kenya kuchorwa ama hata kupaka rangi yoyote ile,mabasi mawili yaliochorwa picha yake yamekamatwa na maafisa wa polisi mjini Mombasa Kenya.
Maafisa wa trafiki mjini Mombasa waliyakagua magari hayo na kuyakamata magari yote yaliokuwa yamechorwa picha pamoja na magari yenye madirisha yasioonyesha ndani.
Magari sita yakiwemo mawili yaliokuwa na picha ya Uhuru yalikamatwa,licha ya agizo la rais kuruhusu wamiliki wa matatu kuchora picha katika magari.
Uhuru alikuwa amesema kuwa hatua hiyo itawasaidia vijana kutumia vipaji vyao ili kuweza kujinufaisha kimaisha.
Uchoraji katika magari hayo na muziki ulipigwa marufuku mnamo mwaka 2003 na aliyekuwa waziri wa uchukuzi John Michuki.

No comments:

Post a Comment