TTCL

EQUITY

Saturday, October 11, 2014

King Majuto Ajipanga Kufanya Filamu Na Diamond Na Wema


Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho nchini, King Majuto amesema hivi kariburi alimshawishi Wema Sepetu azungumze na mpenzi wake Diamond Platnumz ili wafanye kazi ya pamoja. 

Mzee Majuto ambaye ni mshindi wa Tuzo za Watu 2014 ya filamu inayopenda, amesema kuwa amemwachia kazi hiyo Wema ili azungumzee na mzee (Diamond). 
"Hivi karibuni nilikuwa na Wema, nimemwambia aongee na Diamond ili tufanye filamu ya pamoja" Amesema Majuto. 
 
Mimi, Wema na Diamond, hata Diamond ninaweza kuzungumza naye sema nimeanza na Wema kwanza, akikubali mtasikia tu. Kwa upande mwingine Majuto amesema ili acheze filamu anahitaji kulipwa shilingi milioni 3. 
Umri unaenda sasa biashara za nisaidie nisaide hakuna, kama unanitaka ili tufanye kazi unatakiwa uandae milioni 3

No comments:

Post a Comment