Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho
nchini, King Majuto amesema hivi kariburi alimshawishi Wema Sepetu
azungumze na mpenzi wake Diamond Platnumz ili wafanye kazi ya pamoja.
Mzee Majuto ambaye ni mshindi wa Tuzo za
Watu 2014 ya filamu inayopenda, amesema kuwa amemwachia kazi hiyo Wema
ili azungumzee na mzee (Diamond).
"Hivi karibuni nilikuwa na Wema, nimemwambia aongee na Diamond ili tufanye filamu ya pamoja" Amesema Majuto.
Mimi, Wema na Diamond, hata Diamond
ninaweza kuzungumza naye sema nimeanza na Wema kwanza, akikubali
mtasikia tu. Kwa upande mwingine Majuto amesema ili acheze filamu
anahitaji kulipwa shilingi milioni 3.
Umri unaenda sasa biashara za nisaidie nisaide hakuna, kama unanitaka ili tufanye kazi unatakiwa uandae milioni 3
No comments:
Post a Comment