MTANGAZAJI wa kituo cha Redio Times, Hadija Shaibu
‘Dida’, juzikati aliamua kutoa siri yake ya moyoni na kuweka wazi juu ya
tabia yake ya kuachika na kupata mume mpya mara kwa mara.
Mtangazaji wa kituo cha Redio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’ akiwa kwenye bethidei ya Rose Ndauka.
Aliweka bayana kwamba anaachika na kupata mwanaume mpya haraka kwa sababu ana shepu ya kalimati (aina ya andazi linalonona).
Mtangazaji wa kituo cha Redio Times, Hadija Shaibu ‘Dida’ akipozi.
“Naomba watu wajue kuwa ukoo wangu, Rose na wenzake wao Mungu
aliwapatia shepu na urefu wa umbo lakini mimi nina shepu ya kalimati na
ndiyo maana napata waume…ingawa kwa leo sina mume wala mchumba,” alisema
Dida alipokuwa kwenye bethidei ya mwigizaji Rose Ndauka iliyofanyika
juzikati katika Ukumbi wa Collesium, Kariakoo, Dar
No comments:
Post a Comment