TTCL

EQUITY

Thursday, November 14, 2013

LEMA PICHA ZAKE ZAKATALIWA, KUTOKANA NA KUTOKUWA NA MAADILI

Mbunge wa Arusha Mjini mheshimiwa  Godbless Lema  jana  alizua  gumzo  kwa  wapiga  kura  wake baada  ya  kuamua   kuzigawa picha  za  kutengeneza  zilizokuwa zikisambazwa katika  mitandao ya Kijamii zikimuonyesha akilawitiwa.
  
Gumzo  hilo  la aina  yake  lilitokea  jana  katika  mkutano wake  uliofanyika katika  viwanja vya Kilombero jijini Arusha.
  
Muda  mfupi  baada  ya  mkutano  huo kuanza, Lema alimuita  Mke wake (Neema) na  kumtaka  azigawe  picha  hizo  kwa  wananchi  ambazo alikuwa ameziprint kwa wingi..
 
Wananchi waliokuwa kwenye mkutano huo walikataa   kupewa picha hizo  na kusema  kuwa   hazina umuhimu wowote  kwao  na  wakamtaka  mbunge  huyo  azichome  moto kwa kuwa wanajua ni za kutengeneza .
   
Baada ya mabishano  ya  dakika  kadhaa, Godbless Lema aliamuru kura zipigwe  kati  ya  wanaosema  wapewe  na  wanaotaka  zichomwe moto .Waliosema picha zichomwe  moto  walishinda.

Baada  ya  kura  hizo,  picha zilichomwa moto na Lema  akawashukuru wapiga kura wake kwa kuonyesha heshima kwake kwa kuzikataa  picha hizo...

No comments:

Post a Comment