TTCL

EQUITY

Saturday, November 16, 2013

KAPUYA, DENTI KIFO NJE NJE

 
Stori: Mwandishi Wetu
Dalili za kifo zipo nje nje, zinajidhihirisha kwa ukaribu zaidi katika maisha ya Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Profesa Juma Athuman Kapuya, sababu kuu ikiwa zigo la tuhuma za kumbaka na kumwambukiza Ukimwi mwanafunzi.
Siyo Kapuya tu, hata mwanafunzi anayedai kubakwa na waziri huyo wa zamani, naye maisha yake siyo salama, kwa hiyo rai imetolewa kwa wote wawili kupewa ulinzi stahiki.

Shahidi muhimu.
 
Tuhuma kuu ni Kapuya kuripotiwa na gazeti pamoja na mitandao kadhaa ya intaneti, akidaiwa kumbaka mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 16 (jina tunalihifadhi), anayesoma Shule ya Sekondari Turiani, Magomeni, Dar es Salaam.
Mwanafunzi huyo amekuwa akinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa alibakwa mara mbili na Kapuya kisha kuambukizwa Ukimwi wakati alipokwenda kumuomba msaada wa ada ya shule kwa sababu yeye ni yatima.

                                                                                   Mh. Juma Kapuya.

KAPUYA NA KIFO
Kapuya, aliye kiongozi mwandamizi wa Tanzania, akiongoza wizara mbalimbali kama vile Elimu, Kazi, Vijana na Ajira, Habari, Utamaduni na Michezo, Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na kadhalika, maisha yake yapo hatarini kwa sababu zifuatazo;
MOSI; Wananchi waliozungumza na Risasi Jumamosi, wamesema kuwa hatari ya kwanza ni SMS ambayo inadaiwa Kapuya aliituma kwa mwanafunzi huyo akimtishia kumuua.
“Kapuya ni kiongozi mwenye heshima kubwa nchini, kukumbwa na tuhuma za kutishia kuua siyo dogo,” alisema Phabian Tarimo ambaye alidai ni jirani wa mwanafunzi huyo na kuongeza:
“Inawezekana kujiepusha na aibu hiyo ya tuhuma za ubakaji au kutishia kuua, akaamua kujiua.”
PILI; Kingine ambacho kinaashiria hatari kwa maisha ya Kapuya ni SMS ya kutishia kujiua ambayo inadaiwa kiongozi huyo alimtumia denti mlalamikaji.
Vyanzo vyetu vinasema, SMS hiyo kutoka kwa Kapuya inasomeka: “Nimewakosea sana, acha nife mie nakunywa sumu nijiue, na nyie mje mnizike.”

Mchangia maoni mmoja wa mtandaoni, Lubelo Issa, alisema: “Kapuya kutamka kujiua siyo jambo dogo, naamini anamaanisha, inabidi familia yake na marafiki zake wawe karibu naye.
“Ikiwezekana hata polisi wawe macho, maana hilo ni kosa la jinai. Kwa mtu mkubwa kama Kapuya kupewa tuhuma nzito kama hizo, ni rahisi kumkatisha tamaa. Ni rahisi kuuona mwisho wake wa kisiasa.
“Hali yake mbele ya familia yake ipoje? Hayo mambo ni mzigo ambao unaweza kumpeleka mbali hadi kufikia hatua ya kujiua.”

DENTI NA KIFO
MOSI; SMS ambayo amedai kutumiwa na Kapuya ni hatari ya kwanza na katika hilo, imeshauriwa na wananchi kwamba denti huyo alindwe usiku na mchana.
“Kapuya amechafuka sana na ikiwa ni kweli zile SMS zimetumwa na yeye, basi yule mtoto achungwe na alindwe kikamilifu. Kapuya amejenga heshima yake kwa miaka mingi, hawezi kukubali kuchafuliwa kienyeji.
“Inawezekana Kapuya akawa na moyo wa subira pamoja na huruma lakini wapo wapambe ambao wanaweza kuchukua hatua ya kumuua yule mtoto kwa sababu amemchafua bosi wao.”
PILI; Sura ya pili ambayo imeangaliwa kuhusu hatari ya maisha ya denti huyo ni kwamba Kapuya anao maadui wa kisiasa ambao wanaweza kutumia mgogoro huo kujifaidisha.
Laura Kamugisha aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook: “Kuna sayansi moja hapa, adui wa Kapuya anaweza kumuwinda huyo mwanafunzi na kumuua ili kuzidi kumuweka Kapuya matatani.
“Leo ikitokea huyo mwanafunzi ameuawa, kila mmoja fikra zake zitaelekezwa kwa Kapuya. Kwa kweli huyu mtoto yupo hatarini, inawezekana Kapuya akampuuza lakini maadui zake wakamuua ili kumkomoa. Mwanafunzi akiuawa, Kapuya atapelekwa mahabusu na baadaye mahakamani.”

SHAHIDI MUHIMU AZUNGUMZA NA RISASI JUMAMOSI
Mrembo (jina tunalo) ambaye ni rafiki wa denti anayedai kubakwa, alisema kuwa ameshangaa kusikia suala hilo limefika kwenye vyombo vya habari kwa sababu huko nyuma yeye alishalisimamia na mambo yakaisha.
“Sijui kuhusu kubakwa, ila … (anataja jina la denti) aliniambia madai yake, nikampeleka kwa mheshimiwa, kusema kweli nilimbana mheshimiwa na fedha zilitoka. Mimi mwenyewe nilipata mgao,” alisema mrembo huyo.
Akaongeza: “Ninavyojua walikubaliana, siyo kubakwa. Na mimi nilimsaidia kumbana mheshimiwa ili ampe pesa. Alikuwa anahitaji pesa ya kwenda kulipa ada shuleni, pesa alipewa.
“Nilianza kuwa mbali naye baada ya kuona amekuwa karibu na wanaharakati. Kuanzia hapo hakunishirikisha kitu, japo tunawasiliana. Hata leo nimeongea naye, ameniambia yupo… (anataja eneo moja, nje ya Dar).
“Kingine ni kwamba wakati namsaidia ishu yake na mheshimiwa alikuwa anasoma Mugabe Sekondari, sijui Turiani alihamia lini. Na kuhusu Ukimwi mimi sijui hilo, ila  natambua kwamba yule mwanafunzi anatumia dawa.
“Hapa lazima niwe mkweli, siwezi kuthibitisha kama kweli ni Ukimwi na kama ni kweli aliyemwambukiza simjui,” alisema.

KAPUYA VIPI?
Juzi, mwandishi wetu alijitahidi kwa kila namna kumpata Kapuya kupitia simu zake tatu za mkononi, mbili za Airtel na moja ya Vodacom lakini hakupatikana.
Mbili hazikuwa zikipatikana lakini moja ilikuwa ikiita bila kupokelewa, ingawa wakati mwingine ilipopigwa ilionesha mwenye simu alikuwa akizungumza, hivyo kuonesha hakutaka kuwasiliana na mwandishi wetu.
Pamoja na kutumiwa SMS inayomuuliza kuhusu tuhuma hizo, bado Kapuya ambaye kwa sasa ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, hakutoa ushirikiano.
Kuhusu mwanafunzi huyo, Risasi Jumamosi linatambua yupo mafichoni na ahadi yetu ni kuendelea kutoa taarifa zaidi kuhusu tukio hilo kupitia magazeti  pendwa ya Global Publishers Ltd.

No comments:

Post a Comment