Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba
 hii leo amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Kamati ya Fedha ya
 Bunge la Finland.
Katika
 mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Luthuli 
Dar es Salaam, wabunge hao wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa 
jitihada inazofanya za kulinda na kuhifadhi mazingira.
Awali,
 akiwakaribisha wabunge hao Waziri Makamba amesema Tanzania inajivunia 
uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na Finland na kuwashukuru  
wabunge hao kwa kufanya ziara hiyo ya kikazi nchini Tanzania.
Waziri
 Makamba amesema Serikali ya awamu ya Tano imejikita zaidi katika 
kuimarisha Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ikiwa ni pamoja na kuandaa 
Mkakati Mkubwa wa Kitaifa wa kupanda miti nchi nzima hususan maeneo kame
 ili kunusuru nchi na athari za mabadiliko ya Tabianchi.
“Hivi
 sasa tuko katika hatua za kuainisha maeneo yatakayopandwa miti hiyo kwa
 kuangalia aina za udongo na miti itakayoweza kuhimili katika maeneo 
husika” Alisisitiza Makamba.
Waziri
 Makamba ameiomba Serikali ya Finland kuendelea kushirikiana zaidi na 
Serikali ya Tanzania ili kufikia malengo endelevu ya Uchumi na maendeleo
 ya Viwanda bila kuathiri Mazingira.
Naye
 Balozi wa Finland Nchini Tanzania Bw Mart Akhtsary aliyeambatana na 
ujumbe wa wabunge kutoka Finland amemhakikishia Waziri Makamba 
kuendeleza na kudumisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira) January 
Makamba akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Wabunge la Finland. 
Wabunge hao wa Kamati ya Fedha wamefanya mazungumzo na Waziri Makamba 
hii leo Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli, Jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment