TTCL

EQUITY

Monday, December 7, 2015

ULEMAVU SIO SABABU YA KUTOTIMIZA NDOTO YA MAFANIKIO YAKO

Model mlemavu ateka hisia za wanamitindo wa kimataifa

Kanya Sesser katika pozi
Kanya Sesser katika pozi

Baadhi ya watu wenye ulemavu katika miili yao wamekuwa ni watu wa kukata tamaa na wengine kujikuta wakiwa ombaomba kutokana na kukosa mahitaji muhimu na hivyo kujikuta wakiwa tegemezi.
Model Kanya Sesser. mwenye umri wa miaka 23 ameonesha kuwa walemavu wanaweza kuushangaza ulimwengu endapo watapata nafasi, na ndio maana mrembo huyo amejikita katika mitindo bila kujali ulemavu alionao.

Kanya Sesser akiwa na mlezi wake baada ya kutengwa na familia yake
Kanya Sesser akiwa na mlezi wake baada ya kutengwa na familia yake

Kanya Sesser katika pozi
Kanya Sesser katika pozi

Kanya Sesser akiwa na mchumba wake Brian Waters
Kanya Sesser akiwa na mchumba wake Brian Waters

Kanya Sesser katika pozi
Kanya Sesser katika pozi

Sesser, mwenye ulemavu wa miguu anayeishi nchini Thailand, amekuwa akijiingizia kiasi kikubwa cha fedha kwa siku kama mwanamitindo kupitia nguo za ndani za wanawake.
Mrembo huyo kutokana na ulemavu aliozaliwa nao wa miguu alijikuta akitengwa na familia yake na hivyo kulelewa na familia nyingine ambapo akiwa na miaka 15 alijiingiza katika mambo ya mitindo.
Sesser, amedai kuwa hajutii kuwa mlemavu na ndio maana ameamua kujikita kwenye mitindo ambapo amedai kuwa ameingia mkataba na makampuni makubwa nchini kama Volcom, Nike na Rip Curl Girl, huko Los Angeles ambapo kwa siku huingiza zaidi ya kiasi cha dola 1000.
Sambamba na hilo mwanamitindo huyo ni mwanariadha na sasa inadaiwa kuwa yupo katika maandalizi ya kushiriki mbio za walemavu zitakazofanyika Korea Kusini mwaka 2018.

No comments:

Post a Comment