TTCL

EQUITY

Saturday, November 29, 2014

YALIYOJIRI BUNGENI: SOMA MAAZIMIO YA MAPENDEKEZO YA KAMATI YA ZITTO YALIVYOPITISHWA HADI SASA 1 - 6!

1. Tunapendekeza kwamba vyombo vinavyohusika viendelee na uchunguzi kubaini jinai, ikithibitika achukuliwe hatua za kisheria...Azimio la kwanza limepita


2. Tundu Lissu: Vyombo viendelee kuchunguza pesa zilizogawiwa na Rugemalira na ikithibitika wachukuliwe hatua. Pendekezo la pili kuhusu Rugemalira, serikali imeweka marekebisho kuhusu uhalali wa pesa za Rugemalira alizogawa, Bunge limeazimia uchunguzi uendelee kufanyika

3. Azimio la 3 limerekebishwa kuwa waliopokea pesa wachunguzwe na kuchukuliwa hatua mahususi kwa mujibu wa sheria

4. Pendekezo la 4. Kamati inazitaka mamlaka kuzitangaza benki za Mkombozi na Stanbic kama asasi za utakatishaji fedha. Azimio la 4 limepita kwamba Kamati inazitaka mamlaka husika ikiwemo benki kuu kuchukua hatua dhidi ya benki zote zilizohusika

5. Azimio la 5:Serikali ipitie upya mikataba yote ya umeme na kutoa taarifa kabla ya kumalizika kwa Bunge la bajeti lijalo

6. Azimio la 6: Limepita kwamba mamlaka husika ziivunje bodi ya TANESCO na kuiunda upya kwa lengo la kuongeza ufanisi

No comments:

Post a Comment