Ligi
Kuu ya Uingereza (EPL) ilikuwa imalizike Jumapili kwa michezo 10
kupigwa lakini katika mchezo wa Manchester United na Bournemouth
uliokuwa ukitaraji kupigwa Old Trafford ulihairishwa kutokana na sababu
za kiusalama.
Sababu
ya kuhairishwa ni kuonekana kwa kitu ambacho kilidhaniwa kuwa ni bomu
la mlipuko hivyo mchezo ukahairishwa ili kuzuia madhara ambayo yangeweza
kujitokeza iwapo bomu hilo lingelipuka hivyo mchezo ukasimamishwa na
mashabiki kutolewa uwanjani kwa usalama ili kuhakikisha hakuna madhara
ambayo yatajitokeza.
Baada ya kufanyika uchunguzi kumeonekana kuwa halikuwa bomu kama ilivyodhaniwa hapo awali.
Kilichokutwa
ni kifaa ambacho kinatumika kufanya mazoezi ili kuonyesha kama wanyama
wanaotumika katika usalama wanauwezo wa kutambua kitu kilichokuwa ni
mlipuko au sio mlipuko.
Inasemekana
kuwa kifaa hicho kiliachwa na moja ya kampuni ambayo ilikuwwa ikifanya
mazoezi karibu na eneo hilo hivyo wakati wakiondoka wakasahau kuchukua
kifaa hicho ambacho baada ya watu wa usalama kukipata walikiharibu kwa
tahadhari kama linaweza kutokea jambo lolote ambalo sio la kiusalama.
Aidha
baada ya taarifa hiyo, tayari kumetolewa taarifa kuwa mchezo wa
Manchester United na Bournemouth utachezwa siku ya Jumanne saa 4 usiku.
No comments:
Post a Comment