TTCL

EQUITY

Tuesday, December 15, 2015

WAZIRI AIPASHA TANESCO JUU YA KUTOKA UMEME TENA NCHNI


Wizara ya Nishati na Madini imewaagiza watendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuhakikisha uzalishaji wa umeme katika Mradi wa Kinyerezi I na Kinyerezi II unakamilika ifikapo mwezi Februari 2016  na kuanza kufanya uzalishaji ilikuongeza kiasi cha nishati ya  umeme kufikia zaidi ya Megawati 100.
Agizo hilo lilitolewa leo na Naibu Waziri, Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medadi Kalemani alipofanya ziara yake katika kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia nishati ya Gesi cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam,hii ni baada ya kuelezwa kuwa kituo hicho kwa sasa kinazalisha 70 Megawati za umeme ambaohautoshelezi kwa matumizi ya watanzania.
“Watanzania wamechoshwa na mgao wa umeme na wanaimani kubwa na uzalishaji wa kituo hiki cha kuzalisha umeme kwa kutumia gesi hivyo wanatarajia umeme wa uhakika katika kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji na kujipatia kipato”,alisema Dkt.Kalemani.

No comments:

Post a Comment